Rais Raisi: Israel ikifanya kosa jengine dogo haitabaki tena
Get link
Facebook
Twitter
Pinterest
Email
Other Apps
-
Apr 24, 2024 02:45 UTC
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran amesema katika kikao na wasomi wa jimbo wa Punjab nchini Pakistan
kwamba iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya kosa jengine dogo na
kuivamia ardhi takatifu ya Iran, hali itakuwa tofauti kabisa na hakuna
ajuaye kama utawala huo utabaki tena.
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran IRIB, akiwa katika siku ya pili ya ziara yake nchini
Pakista, Ebrahim Raisi jana alitembelea Chuo Kikuu cha "GCU" cha Lahore
na kukutana na wasomi wa kielimu na kitamaduni wa jimbo la Punjab.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliieleza hadhara ya wasomi hao
kwamba, taifa kubwa la Iran liliutia adabu utawala wa Kizayuni kwa
jinai ya kushambulia sehemu ya ubalozi wake nchini Syria, kitendo
ambacho ni kinyume cha sheria zote za kimataifa, mikataba na Hati ya
Umoja wa Mataifa na akaongeza kuwa, iwapo utawala wa Kizayuni utafanya
kosa jengine dogo tu, hautabaki tena.
Seyyid Raisi amesema, madai ya Wamagharibi kwamba eti wanatetea haki
za binadamu hayana ukweli, kama yalivyo madai yao ya kuunga mkono
uhuru wa fikra, na akaongeza kuwa, uungaji mkono wa Marekani na
Magharibi kwa mauaji na kujeruhiwa zaidi ya Wapalestina 100,000 katika
Ukanda wa Ghaza ni ithbati ya ukweli kwamba leo hii wavunjaji wakubwa wa
haki za binadamu ni Wamarekani na Wamagharibi, na madai yao ya kutetea
haki za binadamu ni upuuzi tu.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vilevile ameeleza furaha
aliyonayo kwa kutembelea mji wa kihistoria, kiutamaduni na wa kuvutia wa
Lahore na akasema, uhusiano wa Iran na Pakistan, mbali na kuwa ni wa
ujirani, zaidi ni wa kidini, kiutamaduni, kiustaarabu na wa kinyoyo,
ambao umepelekea kuwepo mfungamano usioweza kuvunjika kati ya mataifa
hayo mawili.
Kwa mwaliko rasmi wa Rais wa Pakistan, Rais Ebrahim Raisi wa
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran siku ya Jumatatu alielekea Islamabad, mji
mkuu wa nchi hiyo, akiongoza ujumbe wa ngazi za juu wa kisiasa na
kiuchumi kwa ajili ya ziara ya siku tatu nchini humo.../
Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni Ujumbe unaoongozwa na Marekani hadi sasa umeshindwa kukomesha mashambulizi ya Wayemeni dhidi ya meli za Bahari Nyekundu Kampeni inayoongozwa na Marekani ya kulinda maslahi ya Israel katika Bahari Nyekundu imeongezeka na kuwa "mapambano makali zaidi" ya baharini ambayo Jeshi la Wanamaji limekabiliana nalo tangu Vita vya Kidunia vya pili, kulingana na ripoti ya AP ikiwanukuu makamanda na wataalam wa jeshi la Amerika. Ripoti hiyo inasema Jeshi la Wanamaji la Marekani limechoka baada ya kukabiliana na operesheni za kijeshi za majini zisizokoma za Wanajeshi wa Yemen kwa zaidi ya miezi saba, huku makamanda wakionya kwamba hali hiyo ni hatari kwao. "Sidhani kama watu wanaelewa jinsi tunavyofanya ni hatari na jinsi meli zinavyoendelea kuwa hatarini," Cmdr. Eric Blomberg aliiambia AP ndani ya meli ya kivita ya USS Laboon katika Bahari Nyekundu. &q
China inapaswa kuadhibiwa - mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amedai kuwa Beijing lazima ilipe gharama kwa ajili ya kuisaidia Urusi wakati wa mzozo wa Ukraine Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema China lazima ilipe gharama kwa madai ya kuendeleza kampeni ya kijeshi ya Urusi nchini Ukraine, akisema Beijing "inachochea" mzozo huo kwa kusambaza vifaa vya kielektroniki na vifaa vingine muhimu kwa Moscow. "Ukweli ni kwamba China inachochea mzozo mkubwa zaidi wa silaha barani Ulaya tangu Vita vya Kidunia vya pili," Stoltenberg alisema Jumatatu katika hotuba yake katika Kituo cha Wilson huko Washington. "Wakati huo huo, inataka kudumisha uhusiano mzuri na Magharibi. Kweli, Beijing haiwezi kuwa nayo kwa njia zote mbili. Wakati fulani, isipokuwa China itabadilika, washirika wanahitaji kuweka gharama. Stoltenberg ameishambulia China mara kwa mara tangu mgogoro wa Ukraine ulipoanza Februari 2022, akisema kuwa Beijing ilikuwa ikiiwezesha Urusi kupigana dhidi ya Kiev,
Msemaji wa Brigedi za Al-Qassam Abu Ubaida, - tawi la kijeshi la Hamas, ametangaza kuwakamata wanajeshi wa Israel katika Ukanda wa Gaza. Alisema, katika hotuba yake iliyorekodiwa, kwamba wapiganaji wa Al-Qassam walifanikiwa kuwakamata wanajeshi kaskazini mwa Ukanda wa Gaza kwa "kuwarubuni wanajeshi wa Israel kwenye moja ya handaki." Alisema kwamba hali za wanajeshi waliokuwa kwenye handaki ni kati ya waliofariki, waliotekwa na kujeruhiwa. Abu Ubaida aliendelea: “Mujahidina wetu waliweza kukamata wanajeshi wa Israeli kutoka katika kikosi kilichoko kambi ya Jabalia. Ameongeza kuwa vikosi vya Al-Qassam walifanya makumi ya operesheni dhidi ya wanajeshi wa Israel katika kipindi cha zaidi ya wiki mbili huko Rafah na Beit Hanoun - Erez. Hata hivyo, msemaji wa jeshi la Israel Daniel Hagari alikanusha habari hizo kwenye akaunti yake ya mtandao wa X, akisema: "Ufafanuzi: Hakuna tukio la kuwateka nyara wanajeshi." Jeshi la Israel limeendelea kushambulia kwa mabomu Ukanda wa