Rais Raisi: Israel ikifanya kosa jengine dogo haitabaki tena
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Apr 24, 2024 02:45 UTC
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran amesema katika kikao na wasomi wa jimbo wa Punjab nchini Pakistan
kwamba iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya kosa jengine dogo na
kuivamia ardhi takatifu ya Iran, hali itakuwa tofauti kabisa na hakuna
ajuaye kama utawala huo utabaki tena.
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran IRIB, akiwa katika siku ya pili ya ziara yake nchini
Pakista, Ebrahim Raisi jana alitembelea Chuo Kikuu cha "GCU" cha Lahore
na kukutana na wasomi wa kielimu na kitamaduni wa jimbo la Punjab.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliieleza hadhara ya wasomi hao
kwamba, taifa kubwa la Iran liliutia adabu utawala wa Kizayuni kwa
jinai ya kushambulia sehemu ya ubalozi wake nchini Syria, kitendo
ambacho ni kinyume cha sheria zote za kimataifa, mikataba na Hati ya
Umoja wa Mataifa na akaongeza kuwa, iwapo utawala wa Kizayuni utafanya
kosa jengine dogo tu, hautabaki tena.
Seyyid Raisi amesema, madai ya Wamagharibi kwamba eti wanatetea haki
za binadamu hayana ukweli, kama yalivyo madai yao ya kuunga mkono
uhuru wa fikra, na akaongeza kuwa, uungaji mkono wa Marekani na
Magharibi kwa mauaji na kujeruhiwa zaidi ya Wapalestina 100,000 katika
Ukanda wa Ghaza ni ithbati ya ukweli kwamba leo hii wavunjaji wakubwa wa
haki za binadamu ni Wamarekani na Wamagharibi, na madai yao ya kutetea
haki za binadamu ni upuuzi tu.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vilevile ameeleza furaha
aliyonayo kwa kutembelea mji wa kihistoria, kiutamaduni na wa kuvutia wa
Lahore na akasema, uhusiano wa Iran na Pakistan, mbali na kuwa ni wa
ujirani, zaidi ni wa kidini, kiutamaduni, kiustaarabu na wa kinyoyo,
ambao umepelekea kuwepo mfungamano usioweza kuvunjika kati ya mataifa
hayo mawili.
Kwa mwaliko rasmi wa Rais wa Pakistan, Rais Ebrahim Raisi wa
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran siku ya Jumatatu alielekea Islamabad, mji
mkuu wa nchi hiyo, akiongoza ujumbe wa ngazi za juu wa kisiasa na
kiuchumi kwa ajili ya ziara ya siku tatu nchini humo.../
Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024 Chanzo cha picha, Reuters Dakika 44 zilizopita Wakati 2024 inakaribia kutamatika, Rais wa Urusi Vladimir Putin alifanya mkutano kila mwisho wa mwaka huko Moscow. Mkutano huu wa wanahabari mara nyingi hujulikana kama "maonyesho ya utendaji ya kila mwaka ya Putin." Hata hivyo, Putin anaweza kuwa amepuuza kwa makusudi baadhi ya matukio katika "onyesho la utendaji" la mwaka huu. Hapa, tunarejea nyuma katika matukio matano muhimu yaliyoshuhudiwa katika mwaka huu kwa upande wa Putin. Wakati wa hafla iliyoandaliwa mnamo Desemba 19, rais huyo wa Urusi alihutubia taifa juu ya maswala kadhaa, ikiwemo uchumi wa nchi hiyo, kushuka kwa viwango vya kuzaliana,Ujio wa Donald Trump na vita vya Israel-Gaza, lakini alitumia muda mwingi wa masaa manne na nusu akiangazia uvamizi unaoendelea Ukraine, vita ambavyo vinaingia katika mwaka wake wa tatu, na alitaka kuainisha juhudi za miezi 12 iliyo...
Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni Ujumbe unaoongozwa na Marekani hadi sasa umeshindwa kukomesha mashambulizi ya Wayemeni dhidi ya meli za Bahari Nyekundu Kampeni inayoongozwa na Marekani ya kulinda maslahi ya Israel katika Bahari Nyekundu imeongezeka na kuwa "mapambano makali zaidi" ya baharini ambayo Jeshi la Wanamaji limekabiliana nalo tangu Vita vya Kidunia vya pili, kulingana na ripoti ya AP ikiwanukuu makamanda na wataalam wa jeshi la Amerika. Ripoti hiyo inasema Jeshi la Wanamaji la Marekani limechoka baada ya kukabiliana na operesheni za kijeshi za majini zisizokoma za Wanajeshi wa Yemen kwa zaidi ya miezi saba, huku makamanda wakionya kwamba hali hiyo ni hatari kwao. "Sidhani kama watu wanaelewa jinsi tunavyofanya ni hatari na jinsi meli zinavyoendelea kuwa hatarini," Cmdr. Eric Blomberg aliiambia AP ndani ya meli ya kivita ya USS Laboon katika Bahari Nyekundu. ...
Wanawake 100 wa BBC 2024: Ni nani yuko kwenye orodha mwaka huu? 3 Disemba 2024 BBC imezindua orodha yake ya wanawake 100 mashuhuri duniani mwaka 2024 Miongoni mwao ni Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Nadia Murad, Aliyenusurika ubakaji na mwanaharakati Gisele Pelicot, muigizjai Sharon Stone, Mwanariadha wa Olimpiki Rebeca Andrade na Allyson Felix, muimbaji Raye, msanii Tracet Emin, mwanaharakati wa tabia nchi Adenike Oladosu na mwandishi Rivera Garza. Kutoka kukabiliana na migogoro hatari na mizozo ya kibinadamu huko Gaza, Lebanon, Ukraine na Sudan, hadi kushuhudia mivutano ya kijamii uliyo...