Posts

Showing posts with the label ISRAEL

Haniya: HAMAS haitasalimu amri, itaendeleza muqawama

Image
  Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kundi hilo la muqawama katu halitasalimu amri, bali litaendeleza mapambano yake kwa nguvu zote. Ismail Haniya amesema hayo katika taarifa, akijibu operesheni ya umwagaji damu iliyofanywa na wanajeshi makatili wa Israel dhidi ya kambi ya wakimbiizi ya Nuseirat, katikati mwa Ukanda wa Gaza na kuongeza kuwa: Hatutakata tamaa, tutaendelea kupigania haki zetu za msingi mkabala wa adui mtenda jinai. Wapalestina wasiopungua 210 waliuliwa shahidi na wengine zaidi ya 400 walijeruhiwa juzi Jumamosi katika mashambulizi ya kinyama ya anga ya Israel yaliyolenga kambi ya wakimbizi ya Nuseirat, maeneo ya mashariki ya Deir al-Balah, na kambi za al-Bureij na al-Maghazi katikati mwa Gaza, sanjari na uvamizi wa ghafla uliofanywa na magari mashariki na kaskazini magharibi mwa Nuseirat. Jinai za Wazayuni katika kambi ya Nuseira

Blinken aanza ziara Mashariki ya Kati katika jitihada za kumaliza vita Gaza

Image
  Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Anthony Blinken atawasili katika mji mkuu wa Misri, Cairo, leo, Jumatatu, mwanzoni mwa ziara yake ya nane katika eneo hilo, kujadili juhudi za kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza, na kuendeleza pendekezo la Rais wa Marekani Joe Biden la kuwepo kwa utulivu. Blinken ameratibiwa kukutana na Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi mchana wa leo, kabla ya baadaye kuelekea Israel kukutana na Netanyahu. Vyombo vya habari viliripoti kuwa Blinken atajadili wakati wa mazungumzo yake na Rais Sisi suluhisho ambazo zitaruhusu kufunguliwa tena kwa kivuko cha Rafah kati ya Misri na Ukanda wa Gaza, ambacho kimefungwa kwa mwezi mmoja. Jeshi la Israel lilichukua udhibiti wa upande wa Palestina wa kivuko hicho, likiituhumu Misri kuhusika na kufungwa kwake. Misri ilijibu kuwa madereva wa lori wanaobeba misaada ya kibinadamu kuelekea Ukanda wa Gaza hawajisikii salama wanapovuka vituo vya ukaguzi vya Israel. Ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani itajumuisha pia Qa

Baraza la vita la Israel ni nini na kwanini baadhi ya wajumbe wamejiuzulu?

Image
  Siku ya Jumapili usiku, Baraza la Vita la Israel lilifanya mkutano kwa mara ya kwanza bila mawaziri wawili wa baraza hilo, Benny Gantz na Gadi Eisenkot, ambao walitangaza kujiuzulu kutoka serikali ya dharura mapema usiku huo. Gantz na Eisenkot walijiunga na serikali iliyoundwa na Netanyahu Oktoba 11, kufuatia kuzuka kwa vita, na ikaitwa serikali ya dharura. Gantz na Eisenkot awali hawakuwa sehemu ya serikali kabla ya vita dhidi ya Hamas, na kwa hivyo kujiondoa kwao kutoka serikali ya Netanyahu hakumaanishi kuanguka kwa serikali. Lakini ndio mwisho wa kile kilichoitwa "serikali ya dharura" na serikali inarudi kama ilivyokuwa kabla ya vita. Gantz alitoa wito kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kufanya uchaguzi haraka iwezekanavyo, akisema: "Tunaondoka leo katika serikali ya dharura kwa moyo mzito, na uamuzi wa kuondoka serikalini ni ngumu na mchungu.” Baraza la Vita la Israel ni nini? Chanzo cha picha, REUTERS Maelezo ya picha, Benjamin Netanyahu Ba

Waziri wa vita wa Israel Benny Gantz ajiuzulu katika serikali ya dharura

Image
  Waziri wa vita katika baraza la dharura nchini Israel Benny Gantz amejiondoa serikalini katika ishara ya kuzidisha mgawanyiko kuhusu mipango ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu baada ya mzozo kuhusu Gaza. Akizungumza wakati wa mkutano na wanahabari mjini Tel Aviv Jumapili ambapo alitangaza kujiuzulu, Bw Gantz alisema uamuzi huo ulifanywa kwa "moyo mzito". "Kwa bahati mbaya, Bw Netanyahu anatuzuia kukaribia ushindi wa kweli, ambao ni uhalali wa mzozo unaoendelea," alisema. Akichukuliwa na baadhi ya watu kuwa mgombea anayeweza kuwania mamlaka nchini Israel, Bw Gantz alitoa wito kwa Bw Netanyahu kupanga tarehe ya uchaguzi. Bw Netanyahu alijibu kwa chapisho kwenye X: "Benny, huu sio wakati wa kuacha kampeni, huu ni wakati wa kuungana." Kiongozi wa upinzani Yair Lapid aliunga mkono uamuzi wa Bw Gantz kama "muhimu na sahihi" kwenye mitandao ya kijamii. Mara tu baada ya tangazo hilo, Waziri wa mrengo wa kulia wa Usalama wa Kitaifa Itamar

HAMAS yatoa vipigo vingine vikali kwa wanajeshi vamizi wa Israel

Image
  Brigedi za Shahid Izzuddin Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS zimetangaza kuwa zimeendelea kuviwinda na kuvitwanga kwa makombora vifaru vya utawala wa Kizayuni katika maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza. Katika ripoti yake ya jana Alkhamisi, tawi hilo la kijeshi la HAMAS limetangaza kuwa, limevitwanga na kuviteketeza vifaru vitatu vya Israel aina ya Merkava mashariki mwa mji wa Dayr al Balah katikati mwa Ukanda wa Ghaza, kwa kutumia roketi aina ya Yasin 105. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, wanamapambano wa HAMAS walitega mabomu kwenye handaki moja katika eneo la Tel al Za'rab magharibi mwa mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Ghaza na kuangamiza wanajeshi watano wa Israel walioingia kwenye mtego huo. Vilevile Brigedi hizo za Izzuddin Qassam zimeendelea kuvipiga kwa makombora vitongoji vya walowezi wa Kizayuni vilivyoko karibu na Ukanda wa Ghaza kwa ku

"Netanyahu ni kichaa; kichaa chake hakitibiki, yeye na mkewe na mwanawe"

Image
  Baada ya waziri mkuu wa Israel, kutoa amri ya kuuliwa kwa umati na kujeruhiwa Wapalestina 610 kwa mkupuo mmoja, watu wengi wamesisitiza kuwa Benjamin Netanyahu ana maradhi ya kichaa kibaya cha kunusa damu za watu wasio na hatia. Makala iliyochapishwa na shirika la habari la Mehr inasema kuwa, tangu ulipopandikizwa utawala katili wa Kizayuni katika eneo la Asia Magharibi mwaka 1948, muda wote tumeshuhudia jinai za kutisha na za kiwendawazimu za Wazayuni dhidi ya Wapalestina lakini jinai zinazofanywa hivi sasa na utawala huo pandikizi na katili ni kubwa mno na ni za kutisha kupindukia kiasi kwamba hivi sasa zimezidi kupata nguvu taarifa kuwa waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu anaugua ugonjwa mbaya sana wa wendawazimu.  Katika sehemu yake moja, makala hiyo imemnukuu Ehud Olmert, waziri mkuu wa zamani wa utawala wa Kizayuni akisema kwenye mahojiano maalumu kwamba, kuna baadhi ya maradhi yana

Misri yatoa matamshi ya chuki dhidi ya Israel licha ya mkataba wa amani - Jerusalem Post

Image
  Gazeti la Israel la The Jerusalem Post lilichapisha makala inayokosoa msimamo wa Misri kuhusu vita vya sasa vya Gaza, na kusema kuwa Cairo inachapisha "ujumbe wa chuki dhidi ya Israel" licha ya mkataba wa amani kati ya nchi hizo mbili. Makala iliyoandikwa na Ruth Wasserman Land, naibu balozi wa zamani nchini Misri, ilisema kuwa Misri inatekeleza sera ya nchi mbili, kwa kushirikiana na Israel na wakati huo huo, kueneza ujumbe wenye uadui nayo. Ruth alisema kuwa Misri imetia saini mkataba wa amani na Israel na inajitahidi kuanzisha njia za kibiashara na kushirikiana na Marekani, lakini kwa upande mwingine inatoa ujumbe ambao unachukia Israel kwa raia wa Misri. Alieleza kuwa kwa mtazamo wa Misri, "kuanzishwa kwa taifa la Palestina ilikuwa nguzo ya msingi ya makubaliano ya amani, na kushindwa kufikiwa kwa hili kuliruhusu utawala wa Misri unaoongozwa na Mubarak kujizuia kuimarisha ushirikiano wa pande mbili na Israel katika nyanja za biashara, utamaduni, utalii na mengineyo

Vikosi vya Yemen vyatumia kombora jipya la balistiki dhidi ya Israel

Image
  Vikosi vya Wanajeshi vya Yemen vimetangaza kutumia kombora jipya la balistiki dhidi ya shabaha ya eneo la kijeshi la utawala haramu wa Israel katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu katika operesheni mpya ya kuiunga mkono Palestina. Msemaji wa vikosi hivyo Brigedia Jenerali Yahya Saree alitoa tangazo hilo siku ya Jumatatu. Amesema kombora hilo jipya la balistiki lililotumiwa limepewa jina la "Palestina," na lilivurumishwa katika ngome ya kijeshi ya Israel katika mji wa Um al-Rashrash, ambao pia unajulikana kama Eilat. Jenerali Saree amesema Kombora hilo "limetumika kwa mara ya kwanza," na ameongeza kuwa operesheni hiyo ilitekelezwa kwa mafanikio. Vikosi vya Yemen vimetekeleza operesheni nyingi za kuunga mkono Wapalestina tangu Oktoba mwaka jana, wakati utawala wa Israel ulipoanzisha vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza. Zaidi ya Wapalestina 36,470, wengi wao w

Israel yathibitisha vifo vya mateka wengine wanne huko Gaza

Image
  Jeshi la Israel linasema kuwa limethibitisha vifo vya watu wanne zaidi waliotekwa nyara na Hamas tarehe 7 Oktoba mwaka jana. Linasema wanne hao waliuawa wakiwa pamoja wakati wa operesheni ya Israel huko Khan Younis kusini mwa Gaza, na kuongeza kuwa miili yao ingali inashikiliwa na wanamgambo hao. Wanaume hao walitajwa kuwa ni Muingereza-Muiisrael Nadav Popplewell, 51, Chaim Peri, 79, Yoram Metzger, 80, na Amiram Cooper, 85. Msemaji wa IDF Adm Daniel Hagari alisema taarifa za kijasusi zilizokusanywa katika wiki za hivi majuzi zimehitimisha tathmini hiyo. "Tunatathmini kuwa wanne hao waliuawa wakiwa pamoja katika eneo la Khan Younis wakati wa operesheni yetu huko dhidi ya Hamas," alisema bila kutoa maelezo zaidi. Mwezi uliopita, Hamas ilidai kuwa Nadav Popplewell alifariki dunia katika shambulizi la Israel mnamo mwezi Aprili. Ofisi ya Mambo ya Nje ya Uingereza ilisema inachunguza, lakini hakuna uthibitisho wa kifo chake hadi sasa. Hamas ilitoa video inayowaonyesha wanaume wen

Harakati ya Kiislamu ya Iraq yatelekeza mashambulizi mapya dhidi ya Israel

Image
Katika kukabiliana na hujuma za utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza hususan katika mpaka wa kusini mwa mji wa Rafah, wapiganaji wa Harakati ya Kiislamu ya Iraq wamefanya operesheni mbili tofauti dhidi ya mitambo ya kimkakati ya ardhi za Palestina zilizokaliwa kwa mabavu mwaka 1948 na kupachikwa jina bandia la Israel Katika kukabiliana na hujuma za utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza hususan katika mpaka wa kusini mwa mji wa Rafah, wapiganaji wa Harakati ya Kiislamu ya Iraq wamefanya operesheni mbili tofauti dhidi ya mitambo ya kimkakati ya ardhi za Palestina zilizokaliwa kwa mabavu mwaka 1948 na kupachikwa jina bandia la Israel. Harakati ya Mapambaano ya Kiislamu ya Iraq lilisema kwenye tangazo lake mtandaoni kwamba wapiganaji  wake walifanya shambulio la ndege zisizo na rubani dhidi ya kiwanda cha kusafisha mafuta katika mji wa bandari wa Haifa.  Taarifa hiyo  imesisi

Mawaziri wa Israel watishia kujiuzulu kutokana na mpango wa kusitisha mapigan

Image
Mawaziri wawili wa siasa kali za mrengo wa kulia wa Israel wametishia kujiondoa na kuuvunja muungano unaotawala iwapo Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu atakubali pendekezo la kusitisha mapigano Gaza lililoanzishwa na Rais wa Marekani Joe Biden siku ya Ijumaa. Waziri wa Fedha Bezalel Smotrich na Waziri wa Usalama wa Kitaifa Itamar Ben-Gvir walisema wanapinga makubaliano yoyote kabla ya Hamas kuharibiwa. Lakini kiongozi wa upinzani Yair Lapid ameahidi kuunga mkono serikali ikiwa Bw Netanyahu ataunga mkono mpango huo. Waziri mkuu mwenyewe alisisitiza kuwa hakutakuwa na mapatano ya kudumu hadi uwezo wa kijeshi na uongozi wa Hamas uangamizwe na mateka wote kuachiliwa. Pendekezo la sehemu tatu la Bw Biden litaanza kwa kusitishwa kwa mapigano kwa muda wa wiki sita ambapo Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) litajiondoa katika maeneo yenye wakazi wengi wa Gaza. Mkataba huo hatimaye utasababisha kuachiliwa kwa mateka wote, "kusitishwa kwa uhasama" na mpango mkubwa wa ujenzi mpya wa Gaza. Lak

Mwandamanaji ajifunga minyororo kwenye nguzo ya kufungia magoli kupinga uvamizi wa Israel, Gaza

Image
  Mwandamanaji ajifunga minyororo kwenye nguzo ya kufungia magoli kupinga uvamizi wa Israel, Gaza Chanzo cha picha, SNS Mwandamanaji amejifunga minyororo kwenye nguzo ya kufunga magoli kabla ya mchezo wa kufuzu kwa mashindano ya Euro 2025 kwa Wanawake wa Scotland dhidi ya Israel kwenye uwanja wa Glasgow's Hampden. Mechi hiyo ilicheleweshwa kwa takriban dakika 45 baada ya mwanamume huyo kutumia kufuli nzito kujifunga kwenye eneo la kufunga magoli akipinga operesheni ya kijeshi ya Israel huko Gaza. Pande hizo mbili ziliporejea uwanjani, timu ya Israel ilinyanyua fulana iliyokuwa na ujumbe "Walete Nyumbani" wakimaanisha mateka waliochukuliwa na kundi la Hamas kwenye picha rasmi ya timu. Mchezo huo hatimaye ulianza dakika 45 baadaye kuliko ilivyopangwa, huku Scotland ikishinda mabao 4-1. Mamia ya watu, wengine wakiwa wamebeba majeneza madogo na bendera za Palestina, walikuwa wamekusanyika nje ya lango kuu. Mwandamanaji huyo aliyeingia kwenye uwanja wa taifa hapo awali alikuwa

Hamas yaonyesha kuridhishwa na mapendekezo ya kusitisha mapigano Gaza

Image
 Kundi la Hamas limeonyesha kuridhishwa kwa sehemu na mapendekezo ya Israeli kuelekea usitishwaji wa mapigano kama ilivyotangazwa na rais wa Marekani Joe Biden, ambaye alitoa wito wa kumalizika kwa mapigano ya karibia miezi minane sasa.  Baada ya kauli ya Hamas , Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu , alionekana kutupilia mbali juhudi za rais Joe Biden kuhusu upatikanaji wa amani, akisisitiza kuwa jeshi lake litaendelea na oparesheni zake za kijeshi. Netanyahu anasema wanajeshi wake wataendelea kupigana ilikuwazuia Hamas kutawala katika ukanda wa Gaza suala ambalo anasema iwapo litafanyika litakuwa ni tishio la kijeshi. Waziri Mkuu wa Israeli kwa upande amesisitiza kuendelea na oparesheni za kijeshi katika mji wa Rafah kuwasaka Hamas. © Ronen Zvulun / Reuters Taarifa ya Rais Biden imekuja pia wakati huu wanajeshi

Israel yamaliza mashambulizi ya wiki tatu kaskazini mwa mji wa Gaza

Image
  Vikosi vya Israel vimeondoka Jabalia kaskazini mwa Gaza, baada ya mashambulizi ya wiki tatu eneo hilo ambayo yalishuhudia makumi ya maelfu ya raia wakitoroka. Jeshi lilisema "mamia ya magaidi [wameondolewa]" na kilomita 10 za mahandaki ziliharibiwa wakati wa operesheni hiyo. Picha kutoka Jabalia zinaonyesha uharibifu mkubwa, huku majengo ya orofa mbalimbali yakiwa yameharibiwa au kulipuliwa kwa mabomu. Vikosi vya Ulinzi vya Israel (IDF) vilikuwa vimerejea mjini humo miezi kadhaa baada ya kujiondoa, vikisema kuwa Hamas inajipanga tena huko. Wakati wa operesheni hiyo, miili saba ya Waisraeli waliouawa wakati wa shambulio la Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba na kupelekwa Gaza iligunduliwa na kurejeshwa makwao. Gazeti la Times la Israel lilisema maafisa wa IDF wameelezea mapigano ya Jabalia kama baadhi ya vita vikali zaidi. IDF ilisema Hamas "imegeuza eneo la kiraia kuwa ngome ya mapigano, iliyofyatuliwa risasi kuelekea upande wa wanajeshi kutoka maeneo ya kujihifadhi

Yemen yaapa kutoa jibu la 'kuumiza mno' baada ya shambulio la US na UK kuua makumi ya watu

Image
Yemen imeapa kuwa itatoa jibu la "kuumiza mno" kwa mashambulizi yaliyofanywa na Marekani na Uingereza dhidi ya meneo kadhaa ya taifa hilo la Kiislamu, na kusababisha vifo vya watu wapatao 16 na kuwajeruhi wengine kadhaa. Ali al-Qahoum, mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen, ameiambia televisheni ya al-Mayadeen ya Lebanon: "ni hakika kabisa kwamba Yemen itajibu vitendo vya kichokozi vya Marekani na Uingereza dhidi ya nchi yetu; na muungano wa Marekani na Uingereza hautaweza kuzuia majibu yetu".   Al-Qahoum amebainisha kwa kusema: "Wamarekani na Waingereza lazima wawe wameelewa jinsi mashambulio ya Yemen yatavyokuwa makali. Makombora yetu ya balestiki yanaweza kulenga shabaha tunazotaka baharini na katika maeneo ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu". Ali al-Qahoum Afisa huyo wa Ansarullah ameeleza kuwa Marekani ambayo ni mshi

" Israeli, kwa bahati mbaya tuko kwenye harakati ya kuwa taifa lililolotengwa" - Alon Pinkas

Image
  s Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Netanyahu anakosolewa kwa mwenendo wake wa vita huko Gaza 28 Mei 2024 Zaidi ya miezi saba baada ya mashambulizi ya Oktoba 7 ambayo yalizua vita huko Gaza, maoni ya umma ya kimataifa yanaonekana kuwa ya kugeuka. Mshikamano wa awali ambao Israeli iliupata baada ya shambulio la Hamas umesababisha maandamano makubwa na ukosoaji mkali, hata kutoka kwa nchi washirika wa jadi. Mateka wengi wa Israel waliotekwa nyara na Hamas hawajulikani waliko, wakati viongozi wa kijeshi wa kundi la Kiislamu la Palestina - kama Yahya Sinwar - wamejificha chini ya ardhi ili kuepuka mashambulio makali ya kijeshi yaliyoamriwa na serikali ya waziri mkuu Israel, Benjamin Netanyahu, katika Ukanda wa Gaza. Kwa juu juu, hata hivyo, zaidi ya Wapalestina milioni moja wamekimbia makazi yao na zaidi ya 35,000 wamekufa, kwa mujibu wa mamlaka ya afya ya Gaza, kufuatia mashambulizi ya Israel ambayo yamesababisha sehemu kubwa ya Ukanda wa Gaza kuwa magofu.

Wako wapi watu 13,000 waliopotea Gaza wakati wa mashambulizi ya Israel?

Image
  Israel? Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Saa 3 zilizopita Wakati idadi ya watu waliouawa huko Gaza inaendelea kuongezeka, idadi hii haijumuishi waathiriwa wapatao 13,000 ambao wamepotea. Wengi wao wamefunikwa chini ya vifusi, lakini mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema wengine huenda wamechukuliwa kwa nguvu. Ahmed Abu Duke amekuwa akimtafuta kaka yake Mustafa kwa miezi kadhaa. Familia hiyo ilikuwa imejihifadhi katika eneo la Hospitali ya Nasser, katika mji wa kusini wa Khan Yunis, wakijaribu kuepuka mashambulizi ya Israel. Lakini walipopata habari kwamba nyumba yao, imeteketezwa na moto, Mustafa alikwenda kuangalia sehemu ya mabaki ya nyumba na mali. Ila hakurudi tena. "Tulitafuta kila sehemu," anasema Ahmed, akielezea eneo palipokuwa na nyumba, sasa kuna mabaki ya vitu vyeusi vilivyoungua. "Eneo la jirani limeharibiwa na majengo ya ghorofa yamebomolewa," anasema. Familia ilimtafuta Mustafa, dereva mstaafu wa gari la wagonjwa, miongoni mwa miili a

"Vitisho vya nyuklia vya Israel vitabadilisha mlingano wa usalama katika eneo"

Image
Katibu wa Baraza la Kistratajia la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesema vitisho vinavyotolewa na maafisa wa utawala wa Kizayuni wa Israel vya kutumia silaha za nyuklia huenda vikawalazimisha wengine kuangalia upya sera zao za nyuklia katika eneo la Asia Magharibi. Sayyid Abbas Araqchi alisema hayo jana katika warsha iliyoandaliwa na kanali ya televisheni ya al-Jazeera ya Qatar mjini Doha, chini ya kaulimbiu 'Mlingano baada ya Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa katika kiwango cha kieneo.' Amebainisha kuwa, maafisa wapenda vita wa utawala wa Kizayuni si tu wanabwabwaja na kutoa vitisho kuhusu kutumia mabomu ya atomiki, lakini si baidi wakaisukuma Tel Aviv itekeleza kivitendo vitisho hivyo. Araqchi ameuambia mkuatano huo mjini Doha kuwa, Israel haijawahi kukiri au kukanusha madai kuwa inamiliki silaha za nyuklia, na hilo linaonesha namna utawala huo una sera fiche na zisizoeleweka. "

Wapalestina 35 wachomwa moto wakiwa hai katika shambulio la kinyama la Israel Rafah

Image
  Jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel limeshambulia kwa makombora kambi ya watu waliolazimika kuhama makazi yao na kuhamia eneo lililotengwa kuwa na usalama huko Rafah, na kuwaua shahidi Wapalestina 35, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto. Shambulio hilo la linyama la jeshi la Kizayuni katika eneo la Tal as-Sultan limefanywa wakati askari wa jeshi hilo wakishambulia pia kwa makombora makazi ya Wapalestina waliokimbia makazi yao katika maeneo ya Jabalia, Nuseirat na mji wa Ghaza na kuua watu wengine 160 katika muda wa saa 24 zilizopita. Hayo yanajiri huku Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Amnesty International likiitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ichunguze jinai na uhalifu wa kivita uliofanywa katika mashambulizi matatu ya hivi karibuni ya Israel yaliyoua raia 44 wa Palestina, wakiwemo watoto 32. Jeshi la Kizayuni linavyoiteketeza Ghaza Amnesty imesema mashambulizi ha

Dakika 34 zilizopitaMaandamano nchini Israel yataka Netanyahu ajiuzulu

Image
  Maelfu ya Waisraeli waliandamana siku ya Jumamosi, katika miji mbalimbali, dhidi ya serikali ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, wakitaka makubaliano ya kuwarejesha mateka wa Israel huko Gaza, huku familia za mateka zikimtaka Waziri Mkuu wa Israel ajiuzulu. Kulingana na gazeti la Kiebrania Haaretz liliripoti, maandamano hayo yalifanyika “siku chache baada ya kutolewa kwa video inayoonyesha sehemu ya kutekwa nyara kwa ambao walichukuliwa mateka siku hiyo.“ Maandamano hayo yalianza Tel Aviv, Haifa, Jerusalem, Beersheba, na karibu na makazi ya kibinafsi ya Netanyahu huko Caesarea. Polisi wa Israel waliwakamata waandamanaji kadhaa, kulingana na picha zilizosambazwa kupitia mashirika ya habari. Jeshi la Israel limeendelea kushambulia kwa mabomu Ukanda wa Gaza na maeneo ya mji wa Rafah, jana Jumamosi, siku moja baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki kutoa amri inayoitaka Israel kusitisha mashambulizi yake dhidi ya Rafah na kuruhusu misaada ya kibinadamu kuingia. Madaktari wa Kipal