Posts

Showing posts with the label IRAN

HAMAS na Jihadul-Islami zakabidhi rasmi majibu yao kwa mpango wa kusimamisha vita Ghaza

Image
  Harakati kuu za Muqawama na ukombozi wa Palestina za HAMAS na Jihadul-Islami zimetoa jibu rasmi kwa pendekezo linaloungwa mkono na Marekani la kusitisha mapigano Ghaza na kubadilishana mateka kwa wafungwa kwa kuongeza baadhi ya "maoni" kuhusu mpango huo. Hayo yamethibitishwa na wapatanishi wa Qatar na Misri. Katika taarifa ya pamoja ziliyotoa jana Jumanne, Hamas na Jihadul-Islami zimesisitiza kuwa ziko tayari kuzungumzia kwa mtazamo chanya mpango huo na kufikia makubaliano na kwamba kipaumbele chao ni "kusimamishwa kikamilifu" mashambulizi yanayoendelea ya Israel dhidi ya Ghaza. Afisa mwandamizi wa Hamas Osama Hamdan ameiambia kanali ya televisheni ya Al-Mayadeen ya Lebanon kwamba harakati yao "imewasilisha baadhi ya maoni kuhusu pendekezo hilo kwa wapatanishi".  Hamdan amefafanua kuwa majibu ya Hamas yametilia mkazo msimamo kwamba makubaliano yoyote lazima yakomeshe uchokozi wa Wazayuni dhidi ya Wapalestina, yahakikishe wanajesh

Kamanda: Nchi za kigeni zina hamu ya kununua droni za Iran

Image
  Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ni moja ya madola yenye nguvu kubwa za ndege zisizo na rubani (droni) duniani. Brigedia Jenerali Hamid Vahedi alisema hayo alipiotembelea kambi ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Iran katika mji wa bandari wa Bushehr, kusini mwa Iran na kueleza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu imepiga hatua kubwa katika utengenezaji wa ndege za kisasa kabisa zisizo na rubani baada ya Ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979, licha ya vikwazo vya maadui. Kamanda Vahedi ameashiria hatua kubwa zilizopigwa na Jamhuri ya Kiislamu katika sekta ya ulinzi na upanuzi wa ushirikiano wa kijeshi  kati ya Iran, nchi za eneo hili na kimataifa na kusema: Wateja wengi wa kigeni wana hamu ya kununua droni za Iran.  Ameeleza bayana kuwa, uuzaji nje wa zana za kijeshi za Iran umeongezeka pakubwa katika miaka ya karibuni na kuongeza kwa kusema, Tehran ina uwe

Tehran yalaani taarifa ya chuki dhidi ya Iran iliyotolewa na marais wa Marekani na Ufaransa

Image
  Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amesema kuwa, yaliyomo katika taarifa ya chuki dhidi ya Iran iliyotolewa na marais wa Marekani na Ufaransa hayana msingi wowote bali yana malengo na misukumo ya kisiasa na ni mwendelezo wa siasa zilizoshindwa tangu zamani. Kwa mujibu wa shirika la habari la IRNA, Nasser Kan’ani Chafi, amelaani taarifa ya pamoja ya marais wa Marekani na Ufaransa, ambayo katika sehemu yake moja ina tuhuma zisizo na msingi na zisizokubalika dhidi  ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Iran yalaani taarifa ya chuki ya marais wa Marekani na Ufaransa dhidi ya Tehran Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza kuwa, nafasi inayojulikana sana ya Tehran katika kusimamisha na kuimarisha uthabiti na usalama katika eneo hili na duniani kiujumla pamoja na kupambana na magenge ya kigaidi kwa shabaha ya kuimarisha usalama wa kimataifa ni jambo lisiloweza kukanushika na kufaf

Kampeni za uchaguzi wa rais wa kabla ya wakati wake zaanza rasmi nchini Iran

Image
  Siku ya kwanza ya kampeni za uchaguzi wa kabla ya wakati wake zimeanza leo rasmi hapa nchini Iran kwa wagombea kupewa muda sawa wa kutangaza sera zao katika kanali mbalimbali za redio na televisheni ya taifa. Kwa mujibu wa Kanali ya Sahab, walioidhinishwa kugombea katika uchaguzi huo wa 14 wa rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Sheria wa Iran, Mostafa Pourmohammadi, Waziri wa zamani wa Afya, Massoud Pezeshkian na Amirhossein Ghazizadeh-Hashemi, Mkuu wa Wakfu wa Masuala ya Mashahidi na Maveterani. Wengine waliopasishwa kugombea nafasi hiyo iliyobaki wazi baada ya kufa shahidi Rais Sayyid Ebrahim Raisi katika ajali ya helikopta Mei 19 mwaka huu, ni Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge), Mohammad Baqer Qalibaf, Meya wa jiji la Tehran, Alireza Zakani, na Saeed Jalili, mjumbe mkuu wa zamani wa mazungumzo ya nyuklia ya Iran. Kwa mujibu wa kifungu c

Iran yatangaza wagombea wa uchaguzi wa urais

Image
 Iran yafichua wagombea wa uchaguzi wa urais Wahafidhina na wapenda misimamo mikali wanatawala orodha ya wanaowania kumrithi marehemu Ebrahim Raisi. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iran imetoa orodha ya mwisho ya wagombea sita watakaochuana katika uchaguzi wa rais wa mwezi huu. Uchaguzi huo uliitishwa baada ya Rais Ebrahim Raisi kuuawa katika ajali ya helikopta mwezi Mei. Wagombea hao waliidhinishwa na Baraza la Walinzi la Iran, jopo la maulama na wanasheria ambao wana mamlaka ya kura ya turufu juu ya sheria iliyopitishwa na bunge, na kuamua ni nani anayeweza kushika nyadhifa katika Jamhuri ya Kiislamu. Masoud Pezeshkian, Mostafa Pour Mohammadi, Saeed Jalili, Alireza Zakani, Amirhossein Qazizadeh Hashemi, na Mohammad Bagher Ghalibaf watashiriki katika uchaguzi wa Juni 28, wizara ilitangaza Jumapili. Ghalibaf ndiye spika wa sasa wa bunge la Iran. Akiwa mkuu wa polisi wa zamani, aligombea urais bila mafanikio mwaka 2005 na 2013. Hashemi kwa sasa anahudumu kama makamu wa rais, wakati Zakani n

Al Houthi: Jeshi la Yemen litaendelea kushambulia manowari kubwa ya kivita ya Marekani

Image
  Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen ameapa kwamba Jeshi la nchi hiyo litaendelea kulenga meli kubwa ya kivita ya Marekani yenye uwezo wa kusheheni ndege za kivita ijulikanayo kama USS Dwight D. Eisenhower. Hadi sasa Jeshi la Yemen limeishambulia manowari hiyo ya kisasa ya Marekani mara mbili katika operesheni za kujibu uchokozi wa Marekani dhidi ya Yemen na pia kuwaunga mkono Wapalestina wa Ukanda wa Gaza ambao wanakabiliwa na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel kwa himaya kamili ya Marekani. Abdul-Malik al-Houthi alisema katika hotuba yake siku ya Alhamisi kwamba "Manowari ya Marekani yenye kusheheni ndege za kivita, 'Eisenhower' itasalia kuwa shabaha ya wanajeshi wa Yemen wakati wowote fursa inapotokea,". Manoari hiyo ililengwa na vikosi vya Yemen katika Bahari ya Sham siku ya Ijumaa na kisha Jumamosi. Vikosi vya Marekani na Uingereza vimeku

UN yathibitisha kukamatwa kwa wafanyakazi wake 11 na waasi wa Houthi nchini Yemen

Image
  Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuachiliwa mara moja kwa wafanyakazi wake 11 ambao wamezuiliwa na vuguvugu la Houthi nchini Yemen. Wafanyakazi hao walichukuliwa katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo yenye migogoro, katika kile kinachoonekana kuwa msako. Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stéphane Dujarric alisema chombo hicho cha dunia kinafuatilia njia zote ili kupata kuachiliwa kwao kwa usalama na bila masharti haraka iwezekanavyo. Kundi hilo lenye silaha linajiona kama sehemu ya "mhimili wa upinzani" unaoongozwa na Iran dhidi ya Israel, Marekani na Magharibi kwa upana, na limetangaza uungaji mkono wake kwa Wapalestina katika Ukanda wa Gaza. Wahouthi wamekuwa wakilenga meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu na kusababisha mashambulizi ya kulipiza kisasi ya anga ya Marekani na washirika wake. Wafanyakazi kadhaa wa mashirika mengine ya kimataifa pia walizuiliwa, ripoti zilizonukuu maafisa kutoka serikali inayotambulika kimataifa ya Yemen zilisema. Simu na kompyu

IRGC Yaapa kulipiza kisasi kwa Israeli baada ya Kifo cha Mshauri wake nchini Syria

Image
IRGC yaapa kulipiza kisasi kwa Israeli baada ya kifo cha mshauri nchini Syria TEHRAN (Tasnim) - Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu alionya utawala wa Kizayuni utalazimika kulipa gharama ya kuuawa shahidi mshauri wa kijeshi wa IRGC katika shambulio la hivi karibuni katika Aleppo ya Syria. Katika ujumbe wake siku ya Jumatano, Kamanda wa IRGC Meja Jenerali Hossein Salami alitoa salamu za rambirambi kwa kuuawa shahidi mtumishi wa IRGC Saeed Abyar aliyeaga dunia katika shambulio la hivi karibuni la anga la utawala wa Israel huko Aleppo nchini Syria ambako alikuwa katika ujumbe wa ushauri. “Wahalifu wa Kizayuni wauaji watoto wanapaswa kukumbuka kwamba watalipa gharama ya damu safi iliyomwagwa katika uhalifu huu. Wao (Wazayuni) wanapaswa kusubiri majibu (ya Iran)," kamanda huyo alisema. Akitoa pongezi kwa marehemu askari wa IRGC kwa msaada wake kwa makundi ya upinzani dhidi ya Israel, jenerali huyo alisema shahidi huyo atawatia moyo vijana wa mapinduzi milele. Utawala w

Mafanikio ya kihistoria ya kudumu ya Shahid Raisi aliyekufa shahidi na wenzake, katika sekta ya mafuta na gesi

Image
Tangu kuingia madarakani serikali ya awamu ya 13, miradi mikubwa 132 ambayo ilikuwa haijakamilika yenye thamani ya dola bilioni 28.5 imekamilika katika sekta ya mafuta na gesi, na wakati huo huo kuanza utekelezaji wa miradi mipya 50 yenye thamani ya dola bilioni 47.5. Kufuatia kidiplomasia hai ya serikali ya 13 katika kuendeleza uhusiano na nchi tofauti na sio za Ulaya na Marekani pekee, uzalishaji na uuzaji nje mafuta ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ulianza mwenendo unaokua tangu mwaka 2021 ambapo hivi sasa Iran inauza nje mapipa milioni 1.5 ya mafuta kwa siku. Katika umri wake wa siku 1000 serikali ya awamu ya 13 imeweza kuongeza uzalishaji wa mafuta kwa asilimia 63 kwa siku ambapo kufuatia juhudi zake kubwa za kutafuta masoko na kuimarisha kidiplomasia ya nishati, imeweza kuandaa uwanja mzuri wa kushirikiana na nchi nyingine katika nyanja za mafuta, uuzaji mafuta, bidhaa za mafuta, bidhaa

Zohreh Elahian, mwanamke wa kwanza kujiandikisha kuwania urais Iran 2024

Image
  Mbunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Zohreh Elahian amekuwa mwanamke wa kwanza kujiandikisha kugombea uchaguzi wa mapema wa duru ya 14 ya urais wa Jamhuri ya Kiislamu, kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raisi katika ajali ya helikopta. Mohsen Eslami, Msemaji wa Makao Makuu ya Uchaguzi ya Iran amesema watu 23 walifika katika ofisi zao zilizoko katika Wizara ya Mambo ya Ndani kwa ajili ya kujiandikisha kuwania nafasi ya urais jana Jumamosi, lakini wanane tu ndio waliopasishwa. Mbali na mwanamama Zohreh Elahian, wengine walioidhinishwa kugombea kiti cha rais hapa nchini hiyo jana ni pamoja na Mbunge wa jiji la Tabriz, Masoud Pezeshkian, na Vahid Haghanian, msaidizi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na ambaye pia amewahi kuwa Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC). Wengine waliodhinishwa jana kugombea kiti cha urais katika uchaguzi wa mapema wa urais ni Meya wa jiji la Tehran, Alireza Zakani, Mbunge wa

Yemen yalenga kwa makombora meli kubwa ya kivita ya Marekani, USS Eisenhower, katika Bahari ya Sham

Image
Msemaji wa jeshi la Yemen amesema wanajeshi wa nchi hiyo wameilenga meli kubwa ya kivita ya Marekani yenywe uwezo wa kubeba ndege, USS Dwight D. Eisenhower, katika Bahari ya Sham ikiwa ni katika kujibu mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu. Brigedia Jenerali Yahya Saree msemaji wa Majeshi ya Yemen alitangaza Ijumaa kupitia televisheni kwamba: "Vikosi vya makombora na wanamaji vya Wanajeshi wa Yemen vimefanya operesheni ya pamoja ya kijeshi iliyolenga meli ya kivita ya Marekani yenye kusheheni ndege, USS Eisenhower katika Bahari ya Sham." Ameongeza kuwa: " Alhamdulillah, operesheni hiyo ilifanywa kwa makombora kadhaa ya balestiki, ambayo yalilenga shabaha kwa usahihi." Jeneral Saree amesema hili lilikuwa jibu kwa mashambulizi ya angani ya Marekani na Uingereza katika maeneo kadhaa katika nchi hiyo ya Kiarabu, ambayo alisema ililenga raia katika

Umuhimu na taathira za wimbi jipya la operesheni za vikosi vya Yemeni katika Bahari Nyekundu dhidi ya vikosi vya Marekani

Image
Vikosi vya Yemen vimefanikiwa kutekeleza oparesheni mpya kadhaa dhidi ya meli zinazosindikizwa na manowari za Marekani katika Bahari Nyekundu na ya Mediterania. Yahya Saree, Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza katika taarifa kuwa vikosi vya majini, ndege zisizo na rubani na makombora vya jeshi la Yemen vimefanikiwa kutekeleza operesheni 6 za kijeshi dhidi ya meli 6 katika Bahari ya Mediterania na Bahari Nyekundu (Bahari ya Sham). Akiashiria kwamba mashambulio dhidi ya meli hizo yote yamefanywa kutokana na meli hizo kukiuka sheria inayopiga marufuku meli kuingia katika bandari za Palestina inayokaliwa kwa mabavu, Yahya Saree amesisitiza kwamba operesheni hizo kubwa za jeshi la Yemen zimefanyika kwa ajili ya kulisaidia taifa linalodhulumiwa la Palestina na kukabiliana na jinai za adui Mzayuni dhidi ya wakimbizi wa Kipalestina katika eneo la Rafah. Saree amesema: Meli ya "LAAX" katika

Bagheri: Operesheni ya Ahadi ya Kweli ilitokomeza uwezo bandia wa Israel wa kuzuia hujuma

Image
  Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: "ubunifu na uamuzi wa Iran wa kumtia adabu mchokozi kwa operesheni ya Ahadi ya Kweli umetokomeza na kufuta uwezo hewa na bandia wa kuzuia hujuma na mashambulio wa utawala wa Kizayuni". Ali Bagheri ameeleza hayo katika mkutano wa kimataifa uliofanyika leo hapa mjini Tehran kwa anuani: "Ghaza; Mdhulumiwa Aliye Imara", ambapo mbali na kusisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kuunga mkono harakati za Muqawama katika eneo amesema: leo hii, Ghaza iliyo imara na inayodhulumiwa ndiyo suala muhimu zaidi kwa ulimwengu. Bagheri amesema, Muqawama wa Kiislamu si vuguvugu la kisiasa au kijamii, bali ni suala ambalo chimbuko lake limo ndani ya imani na itikadi ya wananchi wa Palestina na watetezi wa uhuru duniani na akaongeza kuwa: Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa ilikuwa hatua ya mabadiliko makubwa katika

Umoja wa Ulaya wamuwekea vikwazo Waziri wa Ulinzi wa Iran na Walinzi wa Mapinduzi

Image
 EU imechapisha siku ya Ijumaa, Mei 31 katika Jarida Rasmi duru mpya ya vikwazo dhidi ya Iran, na haswa Pasdaran, Walinzi wa Mapinduzi. Kampuni tatu na watu sita wanalengwa. Picha iliyotolewa na Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Jeshi la Iran mnamo Januari 23, 2024 inawaonyesha Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Mohammad Reza Ashtiani na Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran Jenerali Abdolrahim Mousavi (kulia). AFP - - \

Larijani na Jalili wajiandikisha kugombea urais Iran

Image
Zoezi la kujiandikisha kwa ajili ya kuwania urais katika uchaguzi wa mapema mwezi ujao nchini Iran, limeingia siku ya pili leo ambapo wanasiasa mashuhuri wamejiandikisha kuchukua nafasi ya urais kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raeisi katika ajali ya helikopta. Saeed Jalili, mjumbe mkuu wa zamani wa mazungumzo ya nyuklia ya Iran  alikuwa mwanasiasa wa kwanza mwenye uzito kujiandikisha siku ya Alhamisi kwa ajili ya uchaguzi huo. "Maendeleo ya watu wetu na mielekeo ya kimataifa yanaonyesha kwamba tunakabiliwa na fursa ya kihistoria," alisema baada ya usajili huo, akiashiria hapo kukiri maafisa wa Marekani kwamba sera yao ya "mashinikizo ya juu" dhidi ya Iran imeshindwa. Mapema leo Ijumaa pia, spika wa zamani wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Ali Larijani amefika katika Makao Makuu ya Uchaguzi katika Wizara ya Mambo ya Ndani na kujiandikisha kuwania nafasi ya urais. Akizungu

Kamanda wa IRGC: Israel iliweka tayari mamia ya ndege wakati wa operesheni ya Iran

Image
  Kamanda wa ngazi za juu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) amesema utawala wa Kizayuni wa  Israel uliweka mamia ya ndege za kivita katika hali ya tahadhari kwa ajili ya kukabiliana na mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran mwezi uliopita. Brigedia Jenerali Amir Ali Hajizadeh, kamanda wa Kitengo cha Wanaanga cha IRGC alisema Alhamisi kwamba: "Takriban ndege 221 za kivita ziliwekwa katika hali ya tahadhari kuzuia mashambulizi ya Iran." Ikumbukwe kuwa, Jumatatu, Aprili 1, 2024, utawala wa Kizayuni wa Israel ulishambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus katika shambulio la kigaidi lililopelekea kuuawa shahidi washauri saba wakuu wa kijeshi wa Iran. Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Iran aliitaja hatua hiyo ya Israel kuwa ni shambulio dhidi ya ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na ku

Israel iliweka mamia ya ndege za kivita katika hali ya tahadhari kukabiliana na Iran

Image
Kamanda mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) anasema utawala wa Israel uliweka mamia ya ndege za kivita katika hali ya tahadhari kukabiliana na mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran mwezi uliopita. "Takriban ndege 221 za kivita ziliwekwa macho kuzuia mashambulizi ya Iran," Brigedia Jenerali Amir Ali Hajizadeh, kamanda wa Kitengo cha Wanaanga cha IRGC, alisema katika mji wa Qom, kaskazini ya kati mwa Iran siku ya Alhamisi. Mashambulio hayo ya pande nyingi yalishuhudia Vikosi vya Wanajeshi wa Iran vikirusha makumi ya ndege zisizo na rubani na makombora kuelekea maeneo yanayokaliwa mwishoni mwa Aprili 13. Ulipizaji kisasi huo uliopewa jina la Operesheni True Promise, ulisababisha uharibifu mkubwa kwa vituo vya kijeshi vya Israel katika maeneo hayo. Operesheni hiyo ilikuja kujibu hujuma za utawala huo ghasibu dhidi ya majengo ya kidiplomasia ya Iran katika mji mkuu wa Syria Damascus tarehe 1 Aprili. Uchokozi huo ulipelekea kuuawa shahidi majenerali w

UN inakosolewa kwa kutoa heshima zake kwa Rais wa Iran Hayati Ebrahim Raisi

Image
Napenda kuwahakikishia kuwa Umoja wa Mataifa unasimama katika mshikamano na watu wa Iran, anasema Antonio Guterres Baraza kuu la Umoja wa Mataifa limekosolewa Alhamisi kwa kutoa heshima zake kwa rais wa zamani wa Iran, Ebrahim Raisi aliyefariki katika ajali ya helikopta, huku Marekani ikisusia mkutano huo. Kufuatia ukimya wa dakika moja, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alitoa salamu za rambirambi kwa familia za wahanga wa tukio la Mei 19, pamoja na watu wa Iran. “Napenda kuwahakikishia kuwa Umoja wa Mataifa unasimama katika mshikamano na watu wa Iran na katika harakati za kutafuta amani, maendeleo, na uhuru wa kimsingi”, alisema Guterres. “Kwa hiyo, Umoja wa Mataifa utaongozwa na Mkataba wa kusaidia kutambua amani na usalama, maendeleo endelevu na haki za binadamu kwa wote,” aliongeza. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres. Alipoulizwa kuhusu mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa kutoa rambirambi siku chache baada ya kifo cha kiongozi

Usajili wa wagombea wa uchaguzi mapema wa rais wa Iran waanza

Image
Iran leo imezindua mchakato wa siku tano wa usajili kwa watu wanaotarajia kugombea katika uchaguzi wa 14 wa rais kuchukua nafasi ya Ebrahim Raisi aliyekufa shahidi maisha katika ajali ya helikopta mapema mwezi huu. Rais, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian na wengine sita walikufa shahidi Mei 19, wakati helikopta yao ilipoanguka katika hali mbaya yaa hewa ya ukungu katika milima karibu na mpaka wa kaskazini-magharibi mwa nchi. Wagombea wote lazima waidhinishwe na Baraza la Walinzi wa Katiba lenye  wanachama 12. Hicho ni chombo kikuu cha usimamizi wa uchaguzi nchini. Wizara ya Mambo ya Ndani itatangaza majina ya walioidhinishwa tarehe 11 Juni. Kufuatia kufa shahidi Rais Rasi na wenzake, wakuu wa mihimili mitatu ya dola nchini Iran walikubaliana Jumatatu kwamba uchaguzi wa rais wa haraka utafanyika tarehe 28 Juni. Kulingana na ratiba iliyotangazwa na serikali, kampeni z

Ubalozi wa Israel nchini Mexico wateketezwa moto katika maandamano ya kupinga mauaji ya Rafah

Image
Waandamanaji waliokuwa na hasira wameuchoma ubalozi wa utawala haramu Israel katika jiji la Mexico City nchini Mexico wakati wakibanisha malamiko yao kuhusu mauaji ya kimbari yanaotekelezwa na Israel huko Gaza. Waandamanaji wanaounga mkono Wapalestina walishiriki katika "Hatua ya Dharura Kwa Ajili ya Rafah" na walielezea hasira zao mbele ubalozi wa utawala ghasibu Israel. Waandamnaji waliokuwa na hasira walivurumisha mabomu ya kujitengenezea ya Molotov Cocktail katika jengo la ubalozi huo wa Israel. Aidha waandamanaji waliwarushia mawe polisi wa kutuliza ghasia ili kulipiza kisasi baada ya kurushiwa  mabomu yakuwarushia vitoa machozi. Mexico, siku ya Jumanne, iliwasilisha tamko la kujiunga na kesi ya Afrika Kusini dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) ikiishutumu Israel kwa kutekeleza "mauaji ya kimbari" Gaza. Maandamano kama hayo