Al-Qassam: Tumeangamiza na kukamata mateka askari kadhaa wa Kizayuni + Video

 


Abu Obeida, Msemaji wa Brigedi za Izzuddinul-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS ametangaza kuwa, wapiganaji wa brigedi hizo wamekinasa kwa kukiwekea chambo chini ya handaki kikosi cha jeshi la Kizayuni na kufanikiwa kuwaangamiza, kuwajeruhi na kuwakamata mateka askari kadhaa wa jeshi hilo katika eneo la kambi ya Jabalia kaskazini mwa Ukanda wa Ghaza.

Abu Obeidah, ameonyesha mkanda wa video wa operesheni hiyo iliyotekelezwa na Muqawama na kutangaza kuwa jana Jumamosi jioni katika kambi ya Jabalia, wapiganaji wa Kipalestina waliwawekea chambo wanajeshi wa Israel kilichowaingiza kwenye moja ya mahandaki na kufanikiwa kuwaangamiza na kuwajeruhi askari kadhaa, mbali na wengine waliowakamata mateka.
 
Kufuatia kutangazwa habari hiyo ya kukamatwa mateka wanajeshi kadhaa wa utawala huo ghasibu wa Kizayuni huko Ghaza, furaha, nderemo na vifijo vilitawala jana usiku katika miji ya Dura na Sour na kwenye kambi za wakimbizi wa Kipalestina za Ain Al-Hilweh na Nahr al-Bared zilizoko nchini Lebanon na katika kambi zingine kadhaa.
Wanamuqawama wa Al-Qassam

Katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan pia, sauti za Takbira zilisikika kutoka kwenye vipaza sauti vya misikiti zilizowataka pia watu wamiminike mitaani kusherehekea ushindi huo.

 
Japokuwa kama ilivyokuwa huko nyuma jeshi la utawala bandia wa Israel lilikanusha haraka tukio hilo, msemaji wa Izzuddinul-Qassam alitoa mkanda wa video wa operesheni hiyo iliyotekelezwa na wapiganaji wa Muqawama iliyoonyesha pia silaha na zana zilizonaswa kutoka kwa wanajeshi wa Israel.
 
Mwanachama huyo mwandamizi wa Hamas amebainisha pia kuwa tangu wiki mbili zilizopita, makumi ya operesheni za kijeshi zimetekelezwa dhidi ya jeshi vamizi la Kizayuni huko Rafah na Beit Hanoun, wakati jeshi hilo linajaribu kuwaonyesha Wazayuni kwamba "kufukua makaburi" ya maiti za Wapalestina huko Ghaza ni mafanikio ya kijeshi na kimaadili ambayo limepata katika eneo hilo.../

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China