Biden: Ni 'Uzembe' kwa Trump kusema kesi yake ilipangwa

 .

Rais wa Marekani Joe Biden amesema ilikuwa "uzembe" kwa mtangulizi wake, Donald Trump, kuitaja kesi yake kuwa na udanganyifu, siku moja baada ya kupatikana na hatia na kuweka kihistoria nchini humo.

Akizungumzia maoni ya kwanza kwa umma ya Trump kuhusu kupatikana na hatia kwa makosa 34 ya kughushi rekodi za biashara, Bw. Biden alitetea mfumo wa sheria wa Marekani.

"Kanuni ya Marekani kwamba hakuna mtu aliye juu ya sheria ilithibitishwa tena," Bw Biden alisema kuhusu kilichotokea.

Mapema siku ya Ijumaa, Trump alitoa maneno makali kwenye mkutano na wanahabari katika jengo la Trump Tower huko Manhattan, akimtaja jaji kuwa "mpotovu", kesi hiyo ni "uzushi" na "majambazi" wa Democrats.

Maoni ya Bw Biden siku ya Ijumaa alasiri yanawadia mwanzoni mwa mkutano wa waandishi wa habari wa White House ambapo alijadili Mashariki ya Kati na pendekezo jipya la Israel kwa Gaza.

Bw Biden alisema mpinzani wake wa chama cha Republican katika uchaguzi wa rais wa mwezi Novemba alikuwa amepewa "kila fursa" ya kujitetea, na haikuwa sawa kulalamika kwamba mchakato huo haukuwa wa haki.

"Ni uzembe. Ni hatari. Ni kutowajibika kwa mtu yeyote kusema kuwa hii ilipangwa kwa sababu tu hawapendi uamuzi huo," alisema na kuongeza kuwa Trump anakaribishwa kuwasilisha rufaa.

Bw Biden, ambaye amezungumza mara chache sana hadharani kuhusu matatizo ya kisheria ya Trump, alisema mfumo wa sheria ndio "msingi wa Marekani".

"Mfumo wa sheria unapaswa kuheshimiwa na kamwe tusiruhusu mtu yeyote kuubomoa. Ni rahisi tu namna hiyo. Hiyo ndio Marekani. Ndivyo tulivyo," alisema.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo