Naibu waziri wa fedha wa Marekani amewasili Ukrain

 Naibu Waziri wa fedha wa Marekani, Wally Adeyemo

Adeyemo alisema Marekani inapanga kuchukua hatua zaidi ili kuweka shinikizo kwa uchumi wa Russia.

Naibu Waziri wa Fedha wa Marekani Wally Adeyemo amewasili Kyiv siku ya Jumatano kukutana na maafisa wa Ukraine kwa mazungumzo kuhusu kuimarisha vikwazo dhidi ya Russia pamoja na msaada wa kifedha kwa Ukraine.

Alisema Marekani inapanga kuchukua hatua zaidi ili kuweka shinikizo kwa uchumi wa Russia. Uchumi wa Russia umekuwa uchumi wa wakati wa vita, ambapo kila njia ya uzalishaji na viwanda sasa imejikita katika kujenga silaha za kupambana na vita vyao ilivyovichagua na uvamizi hapa Ukraine, Adeyemo alisema Jumatano katika mji mkuu wa Ukraine.

“Tunahitaji kufanya kila tuwezalo ili tufanikiwe baada ya hapo”. Adeyemo amesema kipaumbele cha Hazina ni kupunguza mapato ya Russia na kuizuia Russia kupata bidhaa inazozihitaji ili kuzisaidia ngome zake za viwanda vya ulinzi, ikijumuisha bidhaa za matumizi ya nchi mbili kutoka China.


Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo