Ukraine yapata mafanikio katika vita vingine - kupambana na ufisadi

 .

Ukraine imepambana na ufisadi uliokithiri tangu siku za kwanza za uhuru wake mwaka 1991, na maafisa wa serikali na wanakampeni huru wanasema kuwa vita hivi ni muhimu katika kushinda vita vilivyopo na Urusi.

Wamepata mafanikio fulani. Shirika la Kupambana na Ufisadi la Transparency International linaorodhesha Ukraine katika kiwango chake cha juu zaidi tangu 2006: kwa sasa ni ya 104 kati ya nchi 180 katika Fahirisi yake ya Mitazamo ya Ufisadi.

"Taasisi nyingi za kupambana na rushwa za Ukraine zinaonyesha matokeo mazuri," Andriy Borovyk, mkurugenzi mtendaji wa Transparency International Ukraine, anaiambia BBC.

Kulingana na yeye, moja ya matokeo kama hayo ni kukamatwa kwa mkuu wa Mahakama ya Juu Zaidi wakati huo, Vsevolod Knyazev, kwa mashtaka ya ufisadi mnamo mwezi Mei 2023.

"Hii inaweza kuwa yenye kutoa matumaini kwasababu ukiona mtu amekamatwa, utafikiria mara mbili kabla ya kufanya ufisadi," alisema.

Kumekuwa na watu wengine waliokamatwa wa ngazi ya juu pia, akiwemo waziri wa kilimo Mykola Solsky na afisa wa huduma ya ujasusi ya SBU, Artem Shylo.

Wote watatu wanakana makosa yoyote na wameachiliwa kwa dhamana. Uchunguzi unaendelea.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo