Yemen yaapa kutoa jibu la 'kuumiza mno' baada ya shambulio la US na UK kuua makumi ya watu


  • Yemen yaapa kutoa jibu la 'kuumiza mno' baada ya shambulio la US na UK kuua makumi ya watu

Yemen imeapa kuwa itatoa jibu la "kuumiza mno" kwa mashambulizi yaliyofanywa na Marekani na Uingereza dhidi ya meneo kadhaa ya taifa hilo la Kiislamu, na kusababisha vifo vya watu wapatao 16 na kuwajeruhi wengine kadhaa.

Ali al-Qahoum, mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen, ameiambia televisheni ya al-Mayadeen ya Lebanon: "ni hakika kabisa kwamba Yemen itajibu vitendo vya kichokozi vya Marekani na Uingereza dhidi ya nchi yetu; na muungano wa Marekani na Uingereza hautaweza kuzuia majibu yetu".
 
Al-Qahoum amebainisha kwa kusema: "Wamarekani na Waingereza lazima wawe wameelewa jinsi mashambulio ya Yemen yatavyokuwa makali. Makombora yetu ya balestiki yanaweza kulenga shabaha tunazotaka baharini na katika maeneo ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu".
Ali al-Qahoum

Afisa huyo wa Ansarullah ameeleza kuwa Marekani ambayo ni mshirika mkuu wa Israel na muungaji mkono wa uvamizi unaendelea kufanywa na utawala huo ghasibu katika Ukanda wa Ghaza, haina nia yoyote ya kuzuia mgogoro usisambae katika eneo.

 
Amsema, kama Marekani haina nia ya kupanua wigo wa vita, inapaswa ikomeshe uungaji mkono wake kwa uvamizi wa Israel dhidi ya Ghaza na mzingiro ilioliwekea eneo hilo. Bila ya hivyo, mashambulizi ya Yemen yataendelea, na wigo wake pia utapanuka.../

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo