Hizbullah: Kama Israel inataka kuingia kwenye vita kamili, sisi tuko tayari kwa hilo

 

  • Hizbullah: Kama Israel inataka kuingia kwenye vita kamili, sisi tuko tayari kwa hilo

Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema: "sisi tuko tayari kwa vita kamili na vya pande zote na utawala wa Kizayuni".

Kwa mujibu wa IRNA, Sheikh Naim Qassem, amesisitiza kuwa: hatua yoyote ya Israel ya kupanua vita na Lebanon itasababisha maangamizi na uharibifu kwa utawala huo na kwa Wazayuni kulazimika kuyahama makazi yao katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu.
 
Naim Qassem amebainisha kwa kusema: "katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, tulipewa vitisho mara kadhaa kututaka tuache kupigana vita na Wazayuni, lakini jibu letu lilikuwa ni kwamba kambi ya Lebanon imeungana na kambi ya Ukanda wa Ghaza".
 
Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameeleza pia kuwa: kwa kuzingatia aina ya sasa ya vita inavyopigana na jeshi la Israel, Hizbullah imetumia sehemu ndogo tu ya uwezo wake.

Kuhusu mpango uliopendekezwa na Rais Joe Biden wa Marekani wa kusitisha mapigano katika Ukanda wa Ghaza na kubadilishana mateka, Sheikh Naim Qassem amesema: mapendekezo ya Biden ya kutuliza hali ya mambo hayana maana; na mpango wake ni kwa ajili ya uchaguzi wa hivi sasa nchini Marekani.

 
Ijumaa ya Mei 31, Rais Joe Biden wa Marekani alidai kwamba utawala wa Kizayuni umewasilisha pendekezo jipya la usitishaji vita na kubadilishana mateka na akazitaka pande husika kutopoteza fursa hiyo na kufikia makubaliano juu ya pendekezo hilo; pendekezo ambalo linajumuisha pia kuachiliwa mateka wa Kizayuni na kujengwa upya kwa Ukanda wa Ghaza.
 
Katika miezi michache iliyopita na kufuatia jinai za kutisha za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza na mauaji ya kimbari uliyofanya dhidi ya Wapalestina katika eneo hilo, Hizbullah ya Lebanon imezishambulia ngome za kijeshi ya utawala huo kaskazini mwa ardhi zinazokaliwa kwa mabavu, suala ambalo limezua hofu kubwa kwa walowezi wa Kizayuni wanaoishi katika maeneo hayo.
 
Hadi sasa makumi ya maelfu ya Wazayuni wamevihama vitongoji vilivyoko karibu na mipaka ya Lebanon kwa kuhofia mashambulizi ya Muqawama.../

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China