Hizbullah ya Lebanon yadungua ndege isiyo na rubani ya utawala wa Kizayuni


  • Hizbullah ya Lebanon yadungua ndege isiyo na rubani ya utawala wa Kizayuni

Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon Hizbullah imeidungua ndege isiyo na rubani ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel ndani ya anga ya Lebanon.

Utawala wa Kizayuni hukiuka anga ya Lebanon kila mara na kushambulia maeneo tofauti ya nchi hiyo.
 
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran IRIB, Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa vikosi vya harakati hiyo ya Muqawama vimeiangusha ndege isiyo na rubani ya utawala wa Kizayuni aina ya Hermes 900 katika anga ya Lebanon.
 
Jeshi la utawala wa Kizayuni limekiri kwamba ndege yake moja isiyo na rubani iliyokuwa ikiruka katika anga ya kusini mwa Lebanon imedunguliwa kwa kombora la kutoka ardhini kuelekea angani.

Karibu wiki mbili zilizopita Hizbullah ya Lebanon iliteketeza puto la kisasa zaidi kiteknolojia na la gharama kubwa zaidi la ujasusi la Israel katika shambulio la ndege isiyo na rubani ililofanya kwa kuvuka matabaka tata ya ulinzi wa anga ya utawala wa Kizayuni.

 
Kwa miezi kadhaa sasa, na kufuatia jinai za kutisha za utawala wa Kizayuni na mauaji ya kimbari unayofanya dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza, Hizbullah ya Lebanon imekuwa ikiyalenga maeneo ya kijeshi ya Wazayuni kaskazini mwa ardhi zinazokaliwa kwa mabavu, suala ambalo limewafanya walowezi wa Kizayuni wanaoishi katika maeneo hayo kuingiwa na hofu kubwa, ambapo hadi sasa makumi ya maelfu ya Wazayuni hao wameondoka katika vitongoji vilivyoko karibu na mpaka wa Lebanon kwa kuhofia mashambulizi ya Muqawama.../

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China