Jihadul-Islami: Tunautazama mpango uliopendekezwa na Biden kwa 'jicho la shaka'

 

  • Jihadul-Islami: Tunautazama mpango uliopendekezwa na Biden kwa 'jicho la shaka'

Harakati ya Muqawama ya Jihadul-Islami ya Palestina imesema inautazama kwa jicho la shaka mpango uliotangazwa na Rais wa Marekani kwa ajili ya kuhitimisha vita vya Ghaza.

Taarifa iliyotolewa na Jihadul-Islami kubainisha msimamo wake juu ya mpango uliotangazwa jana na Rais Joe Biden wa Marekani kwa ajili ya kuhitimisha vita vya Ghaza imeeleza kuwa, harakati hiyo inalitazama kwa jicho la shaka pendekezo la rais wa Marekani linalojaribu kuonyesha kwamba serikali ya Marekani imebadilisha msimamo wake.
 
Harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina imesema: "ingali ni wazi kuwa serikali ya Marekani inaupendelea kikamilifu utawala wa Kizayuni, inaficha jinai zake na inashiriki katika uchokozi unaofanya".
Biden na Netanyahu

Taarifa ya Jihadul-Islami imeendelea kueleza: "tutatathmini pendekezo lolote lile kwa njia ambayo itahakikisha kunakomeshwa vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wetu, kulindwa maslahi na haki zao, na kukidhi matakwa ya Muqawama".

 
Sehemu nyingine ya taarifa hiyo imesema, Jihadul-Islami inalitalii pendekezo la rais wa Marekani na kuchukua msimamo wa kitaifa kuhakikisha uvamizi unakomeshwa; na jeshi la Kizayni linaondoka kikamlifu Ukanda wa Ghaza.../
 

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China