Mamake Michell Obama, Marian Robinson afariki dunia

 .

Marian Robinson, mamake Michelle Obama, mkewe rais wa zamani wa Marekani Barack Obama amefariki dunia akiwana umri wa miaka 86.

Katika taarifa rasmi, familia yake imesema kuwa Robinson alifariki Ijumaa asubuhi.

Robinson alionekana sana katika ikulu ya Marekani katika miaka minane ya utawala wa Barack Obama kati ya mwaka 2009 hadi 2017.

Kwa muda mwingi huo alishughulika kuwalea wajukuu zake wawili Malia na Sasha – binti zake Michelle na Barack Obama.

Katika taarifa kwenye mtandao wa X uliofahamika kama twitter zamani, Michelle Obama alimueleza mamake kuwa kama mtu muhimu kwake – "jiwe la singi ambaye siku zote alinisaidia kwa chochote nilichokihitaji".

" Alikuwa kiungo muhimu kwa familia yetu yote na tumesikitika kutangaza kuwa ameafiriki dunia leo," aliandika.

Katika ujumbe tofuati kwenye mtandao huo wa X,Bwana Obama amesema kuwa“ Alikuwepo na atasalia kuwepo Marian Robinson mmoja pekee”.

“Katika huzuni wetu tunapata nguvu kwa zawadi ya maisha yake,” aliongeza. “Na kwa maisha yetu yote tutajaribu kuishi kwa mfano wake.”

Hakuna maelezo zaidi yaliotolewa kuhusu chanzo cha kifo chake.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo