Mashirika na watu mashuhuri waathiriwa na shambulio la kimtandao dhidi ya TikTok

 .

TikTok inasema inashughulikia shambulio la mtandao ambalo lililenga bidhaa mashirika na watu mashuhuri.

Programu ya kushirikisha video, ambayo inamilikiwa na kampuni ya Kichina ya ByteDance, iliambia BBC kwamba idadi "kidogo sana" za akaunti zimeingiliwa.

Iliongeza kuwa inafanya kazi na watumiaji kurejesha ufikiaji wa akaunti zao.

TikTok haikushirikisha maelezo zaidi juu ya wahusika wa shambulio hilo la mtandaoni, au jinsi lilivyotekelezwa.

Moja ya akaunti iliyoathiriwa ilikuwa ya kituo cha habari cha CNN.

"Tumekuwa tukishirikiana kwa karibu na CNN kurejesha ufikiaji wa akaunti na kutekeleza hatua za usalama zilizoimarishwa ili kulinda akaunti yao siku zijazo," msemaji wa TikTok alisema.

"Tumejitolea kudumisha uadilifu wa jukwaa hili na tutaendelea kufuatilia shughuli zozote zisizo za kweli."

CNN haikujibu mara moja ombi la BBC la kutoa maoni.

TikTok ilisema akaunti ya nyota wa televisheni ya kipindi cha moja kwa moja Paris Hilton pia ililengwa, lakini haikuathiriwa.

Hilton, ambaye ana wafuasi zaidi ya milioni 10 kwenye TikTok, ni mtumiaji hai wa jukwaa hilo.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo