Mwandamanaji ajifunga minyororo kwenye nguzo ya kufungia magoli kupinga uvamizi wa Israel, Gaza

 

Mwandamanaji ajifunga minyororo kwenye nguzo ya kufungia magoli kupinga uvamizi wa Israel, Gaza

.

Chanzo cha picha, SNS

Mwandamanaji amejifunga minyororo kwenye nguzo ya kufunga magoli kabla ya mchezo wa kufuzu kwa mashindano ya Euro 2025 kwa Wanawake wa Scotland dhidi ya Israel kwenye uwanja wa Glasgow's Hampden.

Mechi hiyo ilicheleweshwa kwa takriban dakika 45 baada ya mwanamume huyo kutumia kufuli nzito kujifunga kwenye eneo la kufunga magoli akipinga operesheni ya kijeshi ya Israel huko Gaza.

Pande hizo mbili ziliporejea uwanjani, timu ya Israel ilinyanyua fulana iliyokuwa na ujumbe "Walete Nyumbani" wakimaanisha mateka waliochukuliwa na kundi la Hamas kwenye picha rasmi ya timu.

Mchezo huo hatimaye ulianza dakika 45 baadaye kuliko ilivyopangwa, huku Scotland ikishinda mabao 4-1.

Mamia ya watu, wengine wakiwa wamebeba majeneza madogo na bendera za Palestina, walikuwa wamekusanyika nje ya lango kuu.

Mwandamanaji huyo aliyeingia kwenye uwanja wa taifa hapo awali alikuwa amevalia vazi ambalo huenda lilimfanya kudhaniwa kuwa msimamizi.

Aliondolewa kwenye nguzo ya kufungia magoli na kuongozwa kutoka uwanjani na polisi.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China