Mwigizaji arudisha kitabu alichochukuwa maktaba miaka 47 baadaye

.

Ilikuwa ni afadhali kuchelewa kuliko kutorejesha kabisa kitabu alichokipata mwigizaji Uri Geller.

Aligundua hivi majuzi kitabu cha takriban miongo mitano wakati akipekua masanduku katika chumba chake cha kuhifadhia vitu huko Israel.

Alipata kitabu - kuhusu yeye mwenyewe - ambacho alikuwa amechukua kutoka kwa Maktaba ya Umma ya Los Angeles miaka 47 iliyopita.

Bw Geller aliazima kitabu hicho mnamo Januari 1977.

"Ninafungua sanduku na kuanza kutoa vitabu na mbele yangu nikakutana na karatasi ya manjano," aliambia BBC News.

Mwanaume huyo ambaye sasa yuko katika miaka yake ya 70, alisema kwamba aliondoka Israel mwaka 1972 na kuelekea Marekani kushiriki katika majaribio kadhaa yaliyofanywa na CIA kuchunguza uwezo wake wa kiakili.

Kundi la wanasayansi lilimchunguza sana Bw Geller, na kusababisha kuchapishwa kwa jalada lake ‘The Geller Papers’ mnamo mwaka 1976.

Ilijumuisha mkusanyiko wa karatasi za kisayansi zinazoeleza kwa kina uchunguzi na majaribio aliyofanyiwa alipokuwa Marekani.

Kitabu cha Bw Geller, kilinunuliwa sana.

Aliishia kurejea nacho New York lakini "akakisahau kabisa" kukipeleka maktaba.

Alikipata alipokuwa akipekua-pekua masanduku ya kuhifadhia.

Bw Geller aliyejiita mhifadhi, alisema "alifurahi" mno alipokipata kitabu hicho.

"Nilipokiona, jambo la kwanza lililonijia ni: 'Wow, nimepitia mengi sana maishani mwangu," alisema.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo