Polisi wa US wakamata waandamanaji 70 baada ya kuvamia ubalozi wa Israel, San Fransisco

 

  • Polisi wa US wakamata waandamanaji 70 baada ya kuvamia ubalozi wa Israel, San Fransisco

Polisi wa Marekani katika mji wa San Fransisco wamewakamata waandamanaji wapatao 70 wanaotetea na kuunga mkono Palestina baada ya kuingia kwenye ukumbi wa ubalozi mdogo wa utawala wa Kizayuni wa Israel ulioko kwenye mji huo.

Mtandao wa Kimataifa wa Kiyahudi wa Kupambana na Wazayuni, (The International Jewish Anti-Zionist Network) ambao unasema wanachama wake ni wa Kiyahudi, umetangaza kuwa zaidi ya watu100 walishiriki katika maandamano hayo.
 
Kundi hilo lilifunua mabango kwenye ukumbi wa ubalozi huo mdogo wa Israel baada ya kuuvamia, ikiwa ni pamoja na lenye maandishi yanayosomeka: “kufanya mauaji ya kimbari huwafanya Wayahudi wawe na usalama mdogo zaidi; si kwa jina langu!”
Ubalozi mdogo wa Israel uliovamiwa na waungaji mkono wa Palestina

Mmoja wa waandamanaji aitwaye Sarah mwenye umri wa miaka 54 amesema: "tunafanya hivi kwa sababu sisi ni sehemu ya umati unaoongezeka wa watu wanaotaka kukomeshwa mauaji ya kimbari na ambao wako katika mshikamano na Palestina na wana wasiwasi sana kuhusu ushiriki wa serikali ya Marekani katika mauaji ya kimbari yanayotokea".

Zaidi ya Wapalestina 36,470, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, wameshauawa hadi sasa katika vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yaliyoanzishwa na jeshi la utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Ghaza kufuatia operesheni ya kulipiza kisasi ya Kimbunga cha Al-Aqsa iliyotekelezwa na harakati za Muqawama wa Palestina za Ghaza Oktoba 7,2023

Tangu vilipoanza vita hivyo, Marekani imekuwa ikiusaidia na kuuunga mkono utawala wa Kizayuni kwa kuupatia maelfu ya tani za silaha na zana za kijeshi ambazo unazitumia kuteketezea roho za Wapalestina wasio na ulinzi.../

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo