Saa 2 zilizopitaChama cha Zuma chadai kuhesabiwa upya kwa kura
Chama cha Zuma chadai kuhesabiwa upya kwa kura
![.](https://ichef.bbci.co.uk/ace/ws/640/cpsprodpb/vivo/live/images/2024/6/1/4ce19af8-0292-4242-b6e4-d51db77c69be.jpg)
Chanzo cha picha, Getty Images
Chama cha Umkhonto we Sizwe (MK) cha Rais wa zamani Jacob Zuma kimewasilisha malalamishi kwa Tume Huru ya Uchaguzi ya Afrika Kusini (IEC)
Huku 98% ya kura zikiwa zimejumlishwa hadi sasa, MK inashindwa kupata wingi wa kura katika ngazi ya mkoa huko KwaZulu-Natal.
Msemaji wa chama Nhlamulo Ndhlela amesema idadi ya IEC hazilingani na walizokusanya mashinani na hivyo wanataka kuhesabiwa upya kwa kura.
Ndhlela ametoa wito kwa wafuasi wa MK kutofanya vurugu.