Saa 2 zilizopitaChama cha Zuma chadai kuhesabiwa upya kwa kura

 

Chama cha Zuma chadai kuhesabiwa upya kwa kura

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Chama cha Umkhonto we Sizwe (MK) cha Rais wa zamani Jacob Zuma kimewasilisha malalamishi kwa Tume Huru ya Uchaguzi ya Afrika Kusini (IEC)

Huku 98% ya kura zikiwa zimejumlishwa hadi sasa, MK inashindwa kupata wingi wa kura katika ngazi ya mkoa huko KwaZulu-Natal.

Msemaji wa chama Nhlamulo Ndhlela amesema idadi ya IEC hazilingani na walizokusanya mashinani na hivyo wanataka kuhesabiwa upya kwa kura.

Ndhlela ametoa wito kwa wafuasi wa MK kutofanya vurugu.