Kamanda mkuu wa jeshi la Ukraine adai kudhibiti mji wa mpakani wa Sudzha, Urusi

 

Kamanda mkuu wa jeshi la Ukraine adai kudhibiti mji wa mpakani wa Sudzha, Urusi

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Kamanda mkuu wa Ukraine amedai kuwa wanajeshi wa Ukraine sasa wanadhibiti kikamilifu mji wa mpakani wa Urusi wa Sudzha.

Katika video iliyochapishwa kwenye mtandaio wa Telegram, Oleksandr Syrskyi anaonekana akimwambia Rais Volodymyr Zelensky kwamba majeshi ya Ukraine sasa "yamekamilisha" "utafutaji na uharibifu" dhidi ya wanajeshi wa Urusi huko Suzha, mji ndani ya eneo la Kursk.

BBC haina uwezo wa kujitegemea kuthibitisha hili na haijulikani ni sehemu gani hasa ya eneo la Urusi huko Kursk limetekwa na Ukraine.

Hata hivyo, kama tulivyoripoti mapema kidogo, ripoti ya televisheni ya Ukraine iliyorekodiwa ndani ya mji wa Urusi wa Sudzha ilionyesha wanajeshi wa Ukraine wakiondoa bendera ya Urusi kutoka kwa shule moja.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China