Urusi: Hali katika eneo la Belgorod 'ni tete', - Gavana

Gavana wa eneo la mpakani la Urusi la Belgorod ametangaza hali ya hatari, akisema mashambulizi ya makombora ya Ukraine yanaifanya hali kuwa "tete na yenye kusababisha wasiwasi mno".

Vyacheslav Gladkov amesema katika ujumbe kwenye mtandao wa Telegram kwamba mashambulizi ya kila siku ya Ukraine yameharibu nyumba na kuua na kujeruhi raia.

Tangazo lake linawadia siku nane baada ya Ukraine kuanzisha uvamizi wa ghafla nchini Urusi.

Wanajeshi wa Ukraine wamekuwa wakisonga mbele katika eneo la Kursk nchini Urusi, na kamanda mkuu wa Ukraine alidai mapema wiki hii kwamba kilomita za mraba 1,000 za ardhi ya Urusi ziko chini ya udhibiti wao.

Uvamizi huo ulianza Jumanne iliyopita tarehe 6 Agosti, huku wanajeshi wa Ukraine wakiingia katika eneo la Kursk la Urusi kwenye mpaka.

Tangu wakati huo, Urusi inasema Ukraine imeshambulia eneo jingine la kusini - Belgorod - kutoka mpakani.

Makumi ya maelfu ya watu wamehamishwa kutoka mikoa yote miwili.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China