US: Yumkini Iran na Muqawama zikafanya 'mashambulio makubwa' dhidi ya Israel wiki hii

 

  • US: Yumkini Iran na Muqawama zikafanya 'mashambulio makubwa' dhidi ya Israel wiki hii

Marekani imeonya kuwa Iran na Harakati za Muqawama katika eneo zinaweza kufanya "mashambulizi makubwa" dhidi ya utawala wa Israel ya kulipiza kisasi cha mauaji yaliyofanywa mwezi uliopita ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniya.

Msemaji wa Baraza la Usalama wa Taifa la Marekani, John Kirby ameeleza mbele ya waandishi wa habari kuwa ulipizaji kisasi huo unaweza kutokea wakati wowote wiki hii. 
 
Kirby ameongeza kuwa Washington haijawa na uhakika bado mashambulio hayo yatakuwa kuwaje akimaanisha namna ukubwa wa kisasi hicho utakavyokuwa, lakini akaongezea kwa kusema: "tunaendelea kuiangalia hali hii, kwa karibu sana."
 
Tarehe 31 Julai, utawala haramu wa Kizayuni wa Israel ulimuua shahidi Ismail Haniya, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina, HAMAS, pamoja na mmoja wa walinzi wake katika mji mkuu wa Iran, Tehran.

Utawala wa Kizayuni umekuwa ukijipapatua na kukanusha kuhusika na ukatili huo, lakini Jamhuri ya Kiislamu imesisitiza kuwa Tel Aviv inawajibika kikamilifu na imeapa kuwa itatoa jibu kali.

Kushoto: Brigedia Jenerali Ali Shadmani na Netanyahu

Siku ya Jumatatu, Brigedia Jenerali Ali Shadmani, Naibu Mratibu wa Idara ya Khatamul-Anbiya ya Makao Makuu ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) alisisitiza kuwa, ulipizaji kisasi kwa Jamhuri ya Kiislamu kwa utawala wa Kizayuni "uko njiani."

Mauaji ya kigaidi ya Shahidi Ismail Haniya yalifanywa siku moja tu baada ya shambulio la anga la Israel dhidi ya mji mkuu wa Lebanon Beirut yaliyopelekea kuuawa shahidi Fuad Shukr, kamanda mkuu wa Hizbullah na mshauri wa Katibu Mkuu wa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon Sayyed Hassan Nasrullah.

Hizbullah kwa upande wake, nayo pia imeahidi kutoa jibu kali kwa utawala haramu wa Israel la ulipizaji kisasi.

Harakati za Muqawama za Iraq na Yemen nazo pia zimeapa kuwa zitaungana na Iran na Hizbullah katika kulipiza kisasi cha damu ya Shahidi Ismail Haniya na Shahidi Fuad Shukr.../

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China