Uvamizi wa Ukraine nchini Urusi: Tunachojua kufikia sasa

 

Uvamizi wa Ukraine nchini Urusi: Tunachojua kufikia sasa

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Iwapo unajiunga nasi tu, au unahitaji mshikamano, hebu tuangalie baadhi ya matukio ya hivi punde katika vita vya Urusi na Ukraine, wiki moja baada ya uvamizi wa Ukraine ndani ya eneo la Urusi.

  • Takriban watu 200 ambao wamekimbia eneo la Kursk waliwasili Moscow siku ya Jumanne, kulingana na wizara ya dharura ya Urusi.
  • Ukraine imesema sasa inadhibiti karibu kilomita za mraba 1,000 (maili za mraba 386) za eneo la Urusi katika eneo la Kursk.
  • Lakini Taasisi ya Utafiti wa Vita (ISW) inasema Kyiv inaweza kudhibiti karibu kilomita za mraba 800
  • Mapema siku ya Jumanne, mfumo wa ulinzi wa anga wa Ukraine ulidungua ndege 30 zisizo na rubani zilizorushwa na Urusi na asubuhi ya leo ulizuia harakati za raia wa Ukraine ndani ya eneo la kilomita 20 (maili 12) linalopakana na Urusi.
  • Katika kukabiliana na uvamizi wa kushtukiza wa Kursk, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema jana usiku kwamba "Urusi imeleta vita kwa wengine, na sasa vinakuja nyumbani"
  • Wakati Rais wa Urusi Vladimir Putin alisema Kyiv itapokea kile alichokiita "jibu linalofaa"Kama ukumbusho, Urusi ilizindua uvamizi wake kamili wa Ukraine mnamo Februari 2022. Ingawa Ukraine ilianzisha uvamizi hapo awali, ndio mara ya kwanza vikosi vya kawaida vya Ukraine vimetumiwa kwa njia hii.