Macron akiri ilichofanya Ufaransa 1944 kwa askari wa Afrika Magharibi ni "mauaji ya halaiki"
Macron akiri ilichofanya Ufaransa 1944 kwa askari wa Afrika Magharibi ni "mauaji ya halaiki"
Kwa mara ya kwanza, Rais wa Ufaransa ameyatambua mauaji ya wanajeshi wa Afrika Magharibi yaliyofanywa na Jeshi la Ufaransa mwaka 1944 kuwa ni "mauaji ya halaiki. Macron amechukua hatua hiyo kupitia barua aliyoziandikia Mamlaka za Senegal.
Sehemu moja ya barua ya Macron imesema: "Ufaransa lazima itambue kwamba siku hiyo, makabiliano kati ya wanajeshi na wabeba bunduki waliotaka walipwe mishahara yao halali, yalizua mlolongo wa matukio ambayo yalisababisha mauaji".
Rais wa Ufaransa ameongezea kwa kusema: "pia ni muhimu kubainisha, kadiri inavyowezekana, sababu na ukweli uliosababisha janga hili, nimeziomba taasisi zangu zinijulishe maendeleo ya kazi ya Kamati ya Mrejesho wa Ukweli, ambao serikali yako imeamua kuanzisha, chini ya uongozi wa Profesa Mamadou Diouf, ambaye hadhi na sifa zake zinatambuliwa na wote".
Ufaransa ingali ina wanajeshi wapatao 350 katika koloni lake la zamani la Senegal, ambao zaidi wanatoa mchango wa usaidizi.
Alipoulizwa kuhusu uwepo wa askari hao, Faye amedokeza kwamba haitakuwa kitu ambacho Wasenegali wangekitaka.
Amefafanua kwa kusema: "ni wazi kabisa; nadhani ukibadilisha kidogo tu nafasi, utakuwa na wakati mgumu kufikiria kwamba (ikubalike) jeshi jengine, liwe la China, Russia, Senegal, au nchi nyingine yoyote kuwa na kambi ya kijeshi huko Ufaransa".../