Kaimu rais awasili eneo la ajali

Chanzo cha picha, EPA/Yonhap
Kaimu Rais wa Korea Kusini Choi Sang-mok amefika katika eneo la ajali, ofisi ya rais inasema.
Choi alitoa mwelekeo wa kutoa wafanyikazi, huduma ya afya na vifaa vya kusaidia katika juhudi za uokoaji, ofisi inasema.
Serikali itafanya yote iwezayo kusaidia familia zilizofiwa, inaongeza.
Choi aliteuliwa kuwa kiongozi wa muda wa nchi hiyo siku ya Ijumaa baada ya aliyekuwa kaimu rais kuondolewa madarakani kutokana na mzozo wa kisiasa unaoendelea.