Israel inasema inadhibiti eneo la mpaka wa Gaza na Misri
Jeshi la Israel linasema kuwa limechukua udhibiti wa eneo la kimkakati kwenye mpaka kati ya Gaza na Misri, linalojulikana kama Philadelphi Msemaji wa Kikosi cha Ulinzi cha Israel (IDF) alisema kuwa takribani njia za chini kwa chini 20 zinazotumiwa na Hamas kuingiza silaha Gaza zimepatikana huko. Televisheni ya Misri ilinukuu vyanzo vinavyokanusha hilo, na kusema Israel ilikuwa inajaribu kuhalalisha operesheni yake ya kijeshi katika mji wa kusini wa Gaza wa Rafah. Tangazo hilo linakuja wakati wa mvutano mkali na Misri. "Katika siku za hivi karibuni, wanajeshi wa IDF walianzisha udhibiti wa operesheni kwenye Ukanda wa Philadelphi, kwenye mpaka kati ya Misri na Rafah," msemaji wa IDF Rear Admiral Daniel Hagari alisema Jumatano. Alielezea ukanda huo kama "uhai" kwa Hamas, ambapo kundi hilo "liliingiza silaha mara kwa mara katika Ukanda wa Gaza". Bw.Hagari baadaye alisema katika kikao na wanahabari kwamba hangeweza kuwa na uhakika kwamba njia zote zilivuka ha