Brazil: Mwanamke apeleka maiti benki ili kupata saini ya mkopo

 


Mwanamke mmoja nchini Brazili amezua mjadala mkali katika mitandao ya kijamii baada ya kupeleka maiti ya mzee katika benki, akitarajia kupata saini ya mkopo.

Katika video iliyosambazwa mitandaoni mwanamke huyo alionekana akisukuma maiti ya mzee iliyekuwa imevishwa nguo nadhifu na kukalishwa kwenye kiti cha magurudumu hadi kwenye eneo la wateja kuhudumiwa na kujaribu kumfanya atie saini karatasi iliyokuwa mbele yake.

Alimpa kalamu na kujaribu kumuita asaini karatasi hiyo lakini hakuweza kufanya hivyo.

Wafanyakazi wa benki waliotilia shaka ustawi wa mwanamume huyo huko Rio de Janeiro walipiga simu polisi katika hatua iliyomfanya mwanamke huyo kukamatwa kwa madai ya ulaghai.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China