Isfahan - mji wa kimkakati wa Iran ambapo milipuko ilisikika

 


Video zilizotumwa kwa BBC Kiajemi na wakaazi kutoka Isfahan zilionyesha milipuko juu ya mji wa Isfahan nchini Iran.

Mji huu unajulikana kwa majumba yake, misikiti ya vigae na minara, Isfahan - ambapo milipuko ilisikika usiku kucha - pia ni kituo kikuu cha tasnia ya kijeshi.

Ni mji wa tatu kwa ukubwa nchini Iran, unaoitwa "Nesf-e-Jahaan" au nusu ya dunia, uko katikati ya nchi karibu na milima ya Zagros.

Jiji na eneo lake ni makao ya viwanda vya droni na makombora ya balestiki.

Karibu nao kuna kituo cha nyuklia cha Natanz, kituo muhimu zaidi cha mpango wa kurutubisha nyuklia wa Iran.

Jina Isfahan likiwa na mafungamano na vituo vya nyuklia vya Iran, ishara ya shambulio hilo haitapita bila kutambuliwa.

Ikiwa hili lilikuwa shambulio la Israeli inaonekana kuwa serikali ya Benjamin Netanyahu ilikuwa ikituma ujumbe kwa Iran kwamba ina uwezo wa kushambulia maeneo nyeti katika jimbo hilo huku ikijizuia kufanya hivyo katika hatua hii.

Maafisa wa Irani hawakuharakisha kutangaza kwamba vifaa vya nyuklia katika mkoa wa Isfahan "viko salama kabisa". Iran, ambayo haina silaha za nyuklia, inakanusha kuwa inajaribu kutumia mpango wake wa nyuklia wa kiraia kwa ajili ya kutengeneza silaha za nyuklia.

Hata hivyo kuna taarifa zinazokinzana kuhusu kilichotokea usikuhuo. Msemaji wa shirika la anga za juu la Iran Hossein Dalirian alisema ndege "kadhaa" zisizo na rubani "zimefanikiwa kudunguliwa" na kukanusha ripoti kwamba shambulio la kombora lilifanyika.

Baadaye, Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amir-Abdollahian aliiambia TV ya serikali kwamba "ndege ndogo zisizo na rubani" hazijasababisha uharibifu wowote au majeruhi huko Isfahan licha ya ripoti za "vyombo vya habari vinavyoiunga mkono Israel".

g

Baadhi ya vyombo vya habari vya Iran viliripoti milipuko mitatu karibu na uwanja wa ndege wa Isfahan na kambi ya jeshi la anga.

Kamanda mkuu wa jeshi la Iran Abdolrahim Mousavi alihusisha milipuko hiyo na "kurusha mifumo ya ulinzi dhidi ya ndege kwenye kitu kinachotiliwa shaka".

Vyombo vingine vya habari vya Iran na maafisa walisema ndege hizo zisizo na rubani zimerushwa na "watu waliojipenyeza".

Jeshi la anga la Iran lina kambi katika uwanja wa ndege wa Isfahan, ambao unahifadhi baadhi ya ndege zake za kivita za F-14 zilizozeeka.

Iran ilinunua ndege aina za F-14 zilizotengenezwa Marekani kwa mara ya kwanza miaka ya 1970 chini ya Shah na imeweza kuzifanya zipae tangu wakati huo.

Ndio nchi pekee ulimwenguni ambayo bado inaendesha wapiganaji wa umaarufu wa Top Gun.

Isfahan pia aliwahi kushambuliwa na Israel hapo awali. Mnamo Januari 2023 Iran ililaumu Israeli kwa shambulio la ndege isiyo na rubani kwenye kiwanda cha risasi katikati mwa jiji .

Shambulio hilo liliripotiwa kutekelezwa kwa kutumia quadcopters - ndege ndogo zisizo na rubani.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China