Sayyid Hassan Nasrullah asema utawala wa Israel wa 'Kinazi' hautadumu katika eneo
Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuhusu mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Rafah kusini mwa Ukanda wa Ghaza kwamba, jinai hiyo ya kutisha uliyofanya utawala huo ghasibu inapasa iwaamshe na kuwatoa kwenye usingizi wa mghafala watu waliojisahau duniani na walioshindwa kuwa na msimamo.
Sayyid Hassan Nasrullah amesisitiza kwamba watu waliojisahau
na wasio na msimamo duniani wanapaswa kuzinduka kutoka kwenye usingizi
wa mghafala baada ya kuona jinai za kutisha za utawala ghasibu wa
Kizayuni huko Rafah na akaongezea kwa kusema, utawala huo hauna hisia za
utu au misingi ya kimaadili na ni mbaya zaidi kuliko Wanazi.
Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameeleza bayana kuwa jinai za
utawala ghasibu wa Kizayuni dhidi ya wakimbizi wa Kipalestina katika
Ukanda wa Ghaza zinadhihirisha unyama, uhaini na woga ulionao utawala
huo haramu.
Sayyid Hassan Nasrullah amesisitiza kuwa jinai za kutisha
ulizofanya utawala wa Kizayuni wa Rafah zitaongeza kasi ya
kusambaratika utawala huo ghasibu na kwamba utawala huo wa Kinazi
hautadumu kwa namna yoyote katika eneo hili.
Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameongeza kuwa, jamii ya kimataifa haina uwezo na dhaifu katika kukabiliana na jinai za utawala bandia wa Kizayuni na inatosheka tu na kutoa taarifa za kulaani na kuonyesha kwamba inatiwa wasiwasi na yanayojiri.
Wapalestina wanaokaribia 50 wakiwemo wanawake na watoto waliuawa
shahidi na 249 walijeruhiwa katika shambulio la kinyama la makombora
lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel usiku wa manane wa
Jumapili iliyopita lililolenga kambi ya wakimbizi katika mji wa Rafah,
kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
Kulingana na Wizara ya Afya ya Palestina, karibu nusu ya waliouawa
shahidi katika shambulio hilo walikuwa wanawake, watoto na wazee.../