Posts

Korea Kaskazini yaangusha maputo ya taka taka Korea Kusini

Image
Korea Kaskazini imeangusha takriban maputo 260 yaliyokuwa yamebeba taka Kusini, na kusababisha mamlaka kuwaonya wakazi wake kusalia majumbani. Jeshi la Korea Kusini pia lilionya umma dhidi ya kugusa puto nyeupe na mifuko ya plastiki iliyowekwa ndani yake kwa sababu ina "takataka na takataka". Puto hizo zimepatikana katika majimbo manane kati ya tisa nchini Korea Kusini na sasa yanachambuliwa. Korea Kaskazini na Kusini zimetumia puto katika kampeni zao za propaganda tangu Vita vya Korea katika miaka ya 1950. Awali jeshi la Korea Kusini lilikuwa limesema linachunguza iwapo kulikuwa na vipeperushi vyovyote vya propaganda za Korea Kaskazini kwenye puto hizo. Tukio la hivi majuzi linakuja siku chache baada ya Korea Kaskazini kusema italipiza kisasi dhidi ya "kutawanywa mara kwa mara kwa vipeperushi na takataka nyingine" katika maeneo ya mpaka na wanaharakati Kusini. "Marundi ya karatasi taka na uchafu hivi karibuni vitatawanywa kwenye maeneo ya mpaka na ndani ya ROK

Tal al Sultan; Hospitali pekee inayofanya kazi katika mji wa Rafah

Image
Wizara ya Afya ya Gaza imetangaza kuwa ni hospitali moja tu ambayo imebaki inayotoa huduma katika mji wa Rafah kufuatia mashambulizi ya jeshi la utawala wa Kizayuni. Wizara ya Afya ya Gaza jana ilitangaza kuwa, ni hospitali moja tu iliyosalia kwa ajili ya matibabu katika mji wa Rafah baada ya utawala wa kizayuni kuzishambulia kwa makusudi hospitali na vituo vingi vya afya katika mji huo. Hiyo ni hospitali ya Tal al Sultan inayohusika na masual aya uzazi na magonjwa ya wanawake.   Hospitali ya Abu Yusuf al Najjar, zahanati kuu ya Abu Walid, hospitali ya Rafah, hospitali ya utaalamu bingwa wa tiba ya al Kuwait, hospitali ya Indonesia na zahanati ya Tal al Sultan hazifanyi kazi hivi sasa ikiwa ni natija ya kuendelea mashambulizi na mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel katika mji wa Rafah.  Mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni katika mji wa Rafah  Katika muktadha huo mama wa Kip

Donald Trump akiri juu ya udhaifu wa utawala wa Kizayuni

Image
Donald Trump Donald Trump, Rais wa zamani wa Marekani amesema katika mkusanyiko wa Wayahudi wa Marekani kwamba utawala wa Israel umepoteza uwezo wake. Gazeti la Washington Post limetoa ripoti kwamba Donald Trump, Rais wa zamani wa Marekani, amekiri kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel ni dhaifu katika hafla ya kuchangisha fedha ya wafadhili wa Kiyahudi wa Marekani na kusema kuwa, anaunga mkono haki ya Israel ya kuendeleza mashambulizi huko ukanda wa Gaza. Donald Trump, Rais wa zamani wa Marekani na Benjamin Netanyahu Katika miezi ya hivi karibuni wafadhili wa chama cha Republican wamemshinikiza Trump kuchukua msimamo mkali zaidi wa kuunga mkono utawala haramu wa Israel na Waziri Mkuu wa utawala huo, Benjamin Netanyahu. Trump pia amejivunia sera zake kuhusu utawala haramu wa Israeli wakati alipokuwa Ikulu ya White House na kusema kuwa  utawala wa Israeli unahitaji msaada wake sa

Licha ya mauaji ya Rafah, US yasema Israel bado haijavuka 'mstari mwekundu' wa Biden

Image
  Msemaji wa Baraza la Usalama wa Taifa la Marekani John Kirby amedai kuwa Israel haijakiuka "mstari mwekundu" wa Rais Joe Biden wa kuifanya Washington isitishe katika siku za usoni kuipatia Tel Aviv silaha za mashambulizi kwa sababu inavyohisi Marekani Israel haitaanzisha operesheni ya ardhini ya kuuvamia kikamilifu mji wa Rafah wa kusini mwa Ukanda wa Ghaza. Licha ya kutoa kauli ya kulaani mauaji ya halaiki yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni mwishoni mwa wiki katika kambi ya wakimbizi mjini Rafah na yaliyopelekea Wapalestina wapatao 50 kuuawa shahidi na 250 kujeruhiwa, na kuyaelezea mauaji hayo kuwa ni  "ya kusonensha moyo" na "ya kutisha", lakini Kirby amesema Marekani haipangi kufanya mabadiliko yoyote katika sera zake kutokana na vitendo vya Israel. Ameongeza kuwa Marekani inafuatilia matokeo ya uchunguzi unaofanywa na Israel yenyewe kuhusu kile ambacho serik

Sayyid Hassan Nasrullah asema utawala wa Israel wa 'Kinazi' hautadumu katika eneo

Image
  Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuhusu mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Rafah kusini mwa Ukanda wa Ghaza kwamba, jinai hiyo ya kutisha uliyofanya utawala huo ghasibu inapasa iwaamshe na kuwatoa kwenye usingizi wa mghafala watu waliojisahau duniani na walioshindwa kuwa na msimamo. Sayyid Hassan Nasrullah amesisitiza kwamba watu waliojisahau na wasio na msimamo duniani wanapaswa kuzinduka kutoka kwenye usingizi wa mghafala baada ya kuona jinai za kutisha za utawala ghasibu wa Kizayuni huko Rafah na akaongezea kwa kusema, utawala huo hauna hisia za utu au misingi ya kimaadili na ni mbaya zaidi kuliko Wanazi. Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameeleza bayana kuwa jinai za utawala ghasibu wa Kizayuni dhidi ya wakimbizi wa Kipalestina katika Ukanda wa Ghaza zinadhihirisha unyama, uhaini na woga ulionao utawala huo haramu. Sayyid Hassan Nasrullah

Bendera ya Palestina yapepea ndani ya Bunge la Ufaransa

Image
Bendera ya Palestina imepepea katika Bunge la Ufaransa. Kwa mujibu wa gazeti la Ufaransa Le Figaro, Sébastien Delogu, mbunge wa Ufaransa, alinyanyua na kupeperusha bendera ya Palestina kwa muda ndanbi ya Bunge la nchi hiyo wakati wa kipindi cha masuali kwa serikali na kwa mara nyingine tena akaonysha uungaji mkono wake wa dhati kwa piganio tukufu la Palestina. Hatua ya mbunge huyo wa chama cha Unyielding France katika bunge la Ufaransa imechukuliwa sambamba na ukosoaji mkubwa na wa wazi wa wanachama wa chama hicho hasa kiongozi wake mkuu Jean-Luc Melenchon na Manuel Bompard, mwanachama mwingine wa chama hicho. Bendera ya Palestina katika Bunge la Ufaransa Siku ya Jumanne, Jean-Luc Melenchon alionyesha sehemu ya hotuba yake aliyotoa katika mkutano wa Umoja wa Wananchi katika mji wa Besançon mashariki mwa Ufaransa na kutoa wito wa kusimamishwa mara moja utumaji silaha kwa utawala haramu wa  Isra

Nchi iliyosimama juu ya nguzo mbili katikati ya bahari, ambayo pia ina timu yake ya mpira wa miguu

Image
  Chanzo cha picha, Robert Harding/Alamy 9 Februari 2024 Hii ni hadithi ya matukio ya ajabu ambayo yalianza kwa barua pepe. Sitasahau barua pepe hiyo na matukio yaliyofuata. Mnamo Mei, 2020 nilipokea ujumbe kutoka kwa mwanamfalme Michael wa Zealand akielezea nia yake ya kuzungumza nami. Ujumbe huu mmoja ulinivutia kwa ulimwengu wenye historia na jiografia tofauti. Mambo mengi yaliunganishwa nayo, kama vile wafalme walioketi, madai ya ardhi, tofauti za kihistoria, Vita vya Kidunia vya pili, vituo vya redio vya maharamia, kukataza simu. Nilifurahi sana kupokea barua pepe hii. Sijawahi kuwa na mkuu kunitumia ujumbe hapo awali na pengine hatanitumia katika siku zijazo. Sealand ni kisiwa kidogo karibu na pwani ya Suffolk ya Uingereza. Inachukuliwa kuwa nchi ndogo zaidi ulimwenguni. Kwa kweli, ilitumika kama jukwaa la kuzuia ndege wakati wa Vita vya Dunia vya pili. Ilijengwa mnamo 1942 na baadaye ikaitwa HM Fort Ruffs. Ngome iliyo na vifaa vya kutosha na mizinga baharini Ngome hii ik