Rais wa Ukraine ataka anga ya Ukraine kulindwa sawa na ilivyolindwa Israel

 


 

Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky ametoa wito kwa washirika wa Ukraine kuilinda kwa njia sawa na walivyoweza kuilinda Israeli kutokana na shambulio la anga kutoka Iran.

Katika hotuba yake ya Jumatatu jioni, rais huyo wa Ukraine alisema kwamba baada ya shambulio la Iran, "ulimwengu mzima uliona vitendo vya washirika katika anga ya Israel na nchi jirani jinsi umoja wa kweli unaweza kuwa na ufanisi katika kulinda dhidi ya ugaidi ikiwa nia ya kutosha ya kisiasa ni msingi wa umoja.”

"Israel si mwanachama wa NATO, na hakukuwa na haja ya kitu chochote kama kuwezesha Ibara ya 5 [ya Mkataba wa NATO juu ya ulinzi wa pamoja wa wanachama wote wa muungano]. Na hakuna mtu aliyeingizwa kwenye vita. Walisaidia tu kulinda maisha, "Zelensky alisema.

Siku ya Jumapili usiku, Iran ilirusha zaidi ya makombora 300 na ndege zisizo na rubani kuelekea Israel.

Kulingana na wanajeshi wa Israeli na Magharibi, ulinzi wa anga wa Israeli na washirika wake, wakiungwa mkono na ndege za kijeshi kutoka Marekani, Uingereza na Ufaransa, waliharibu 99% ya makombora haya.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo