China yaanza mazoezi ya 'adhabu' kando yaTaiwan

 .

China imeanza mazoezi ya kijeshi kuzunguka Taiwan siku tatu tu baada ya William Lai kuapishwa kama rais mpya wa kisiwa hicho kinachojitawala.

Li Xi, msemaji wa Jeshi la Ukombozi la Watu wa China, ametaja mazoezi hayo kuwa "adhabu kali" kwa "vitendo vya kujitenga".

Mazoezi hayo, yaliyoanza mapema Alhamisi, yanafanyika kuzunguka kisiwa kikuu, ikiwa ni pamoja na Mlango-Bahari wa Taiwan kuelekea magharibi yake, na kuzunguka visiwa vinavyodhibitiwa na Taipei vya Kinmen, Matsu, Wuqiu na Dongyin.

Wizara ya ulinzi ya Taiwan ililaani vitendo vya Beijing, na kuvitaja kuwa "uchochezi ".

Taipei imetuma vikosi vya majini, anga, na ardhini "kutetea mamlaka ya [kisiwa]", wizara iliongeza.

Jeshi la China limesema mazoezi yake yanalenga doria za pamoja za utayari wa kupambana na anga, mashambulizi ya usahihi katika malengo muhimu, na operesheni jumuishi ndani na nje ya kisiwa hicho ili kupima "uwezo wa pamoja wa kupambana" wa vikosi vyake.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo