Kijana muuaji aliyenunua mapanga 79 mtandaoni atajwa jina lake

 .

Jaji wa Mahakama ya Juu ameamua kuwa umma unafaa kuambiwa jina la kijana mfanyabiashara wa dawa za kulevya ambaye alinunua visu 79 na mapanga katika miezi kadhaa kabla ya kumdunga mtu na kumuua.

Bi Justice Foster ameondoa amri ambayo iliwazuia wanahabari kufichua utambulisho wa Rayis Nibeel mwenye umri wa miaka 17, ambaye amepatikana na hatia ya kumuua Omar Khan mwenye umri wa miaka 38 huko Luton.

Amri ilikuwa imetolewa chini ya sheria iliyolenga kuwalinda watoto na vijana wanaohusika katika kesi mahakamani.

Lakini jaji ameondoa amri hiyo baada ya BBC kuhoji kuwa kufichua jina la Nibeel ni kwa manufaa ya umma.

Mapema mwaka huu majaji walikuwa wamempata Nibeel na kijana mwingine, Umer Choudhury mwenye umri wa miaka 18, na hatia ya kumuua Bw Khan, ambaye alishambuliwa kwa kisu cha cha inchi 15 (sentimita 37.5).

Walikuwa wamesikia jinsi Bw Khan, wa Leicester Road, Luton, alivyofariki katika eneo la shambulio katika eneo la Sundon Park eneo la Luton mnamo Septemba 16, 2023, baada ya kuzuka kwa mzozo wa dawa za kulevya.

Bi Justice Foster aliwafunga vijana wote wawili siku ya Ijumaa wakati wa kusikilizwa kwa hukumu katika Mahakama ya St Albans Crown.

Alisema Nibeel, wa Butely Road, Luton, atatumikia kifungo kisichopungua miaka 20 na Choudhury, wa Tulip Close, Luton, kifungo kisichopungua miaka 18.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo