Sunak atangaza uchaguzi mkuu wa Uingereza utafanyika tarehe 4 Julai

 .

Waziri mkuu wa Uingereza Rishi Sunak ameapa "kupigania kila kura" alipokuwa akiitisha uchaguzi mkuu wa mapema wa Uingereza Alhamisi tarehe 4 Julai.

Waziri Mkuu alitoa tangazo hilo katika hotuba yake, wakati akijipigia debe kushinda muhula wa tano kwa wahafidhina.

Hatua hiyo ambayo haikutarajiwa ilibadilisha matarajio ya kura, ambayo inaweza kuwa imewapa wabunge wa chama chaConservative fursa nzuri ya kuziba pengo na chama cha Labour.

Sir Keir Starmer alisema ni "wakati wa mabadiliko" kuondokana na "Machafuko ya chama tawala".

Chama cha Labour kimekuwa kikionyesha kuongoza katika kura za maoni za kitaifa, na kimesisitiza kuwa ina kampeni iliyoandaliwa kikamilifu na tayari kuanza.

Bunge sasa litasitishwa siku ya Ijumaa, kabla ya kufungwa rasmi Alhamisi wiki ijayo kwa kampeni rasmi ya uchaguzi ya wiki tano.

Ina maana kuna siku mbili tu za kupitisha sheria yoyote ambayo imesalia - hatua ambayo itamaanisha kuwa baadhi ya hatua zilizokusudiwa za serikali zitalazimika kuachwa.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo