12 wauawa katika shambulio la bomu la Israel nchini Syria
Shambulio la makombora la Israel katika maeneo ya vijijini ya Aleppo nchini Syria alfajiri ya Jumatatu yamesababisha vifo vya takriban watu 12 na wengine kujeruhiwa, kulingana na Agence France-Presse
Shirika la Agence France-Presse limenukuu Shirika la Kufuatilia Haki za Binadamu la Syria likisema kwamba shambulio hilo la bomu lililenga mji wa Hayyan ulioko magharibi mwa Aleppo
Shirika hilo liliripoti kwamba kulikuwa na "shambulio la anga la Israel kwenye eneo la mji wa Hayyan katika vijiji vya kaskazini mwa Aleppo, ambapo shabaha hiyo ilisababisha milipuko ya mfululizo katika kiwanda cha shaba eneo hilo," ambacho kinadhibitiwa na vikundi vya Iran, na kusababisha kuuawa kwa watu 12 wa vikundi vinavyounga mkono Iran
Israel haijatoi maoni yoyote juu ya shambulio hilo.
Vyombo vya habari rasmi vya Syria vilinukuu chanzo cha kijeshi na kusema kuwa watu kadhaa waliuawa katika shambulio la anga la Israel lililolenga maeneo karibu na mji wa Aleppo nchini Syria siku ya Jumatatu.
Shirika la habari la Reuters linasema hili ni shambulio la pili kuripotiwa nchini humo katika kipindi cha chini ya wiki moja.