Balozi wa Uingereza aondoka baada ya 'kuwanyooshea bunduki wafanyakazi'

 

Balozi wa Uingereza aondoka baada ya 'kuwanyooshea bunduki wafanyakazi'

.

Chanzo cha picha, X/@subdiplomasia

Balozi wa Uingereza nchini Mexico ameripotiwa kuacha wadhifa wake mapema mwaka huu baada ya kumuoteshea bunduki mfanyikazi wa ubalozi wa eneo hilo.

Video iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii, iliyoripotiwa awali na Financial Times, inamuonyesha Jon Benjamin akimwotesha mtu mwingine kwa bunduki huku akitazama chini kwenye silaha hiyo.

Iliandikwa: "Katika muktadha wa mauaji ya kila siku huko Mexico na wafanyabiashara wa dawa za kulevya, anathubutu kutania."

Bw Benjamin bado hajatoa maoni yake kuhusu kile kinachoonekana kuwa mzaha mbaya.

Hakuna tangazo rasmi kuhusu nafasi ya Bw Benjamin ambalo limetolewa na Ofisi ya Mambo ya Nje, Jumuiya ya Madola na Maendeleo ya Uingereza (FCDO).

Lakini hajaorodheshwa tena kama balozi wa Mexico kwenye tovuti rasmi ya serikali, ambayo inasema alikuwa katika wadhifa huo "kati ya 2021 na 2024".

Katika video hiyo, mwanamume anayefanana na Bw Benjamin anaonekana akisongeza silaha karibu na gari hilo, akiwalenga watu tofauti. Kicheko kinaweza kusikika kwa nyuma. Mwanaume mmoja anaonekana akionyesha ishara ya kuwa na wasiwasi kwani silaha hiyo inamlenga yeye.

BBC imewasiliana na Bw Benjamin kutafuta maoni yake.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo