Joto laua zaidi ya watu 50 nchini India kwa siku tatu

 TH

Zaidi ya watu 50 wamefariki dunia nchini India katika muda wa siku tatu zilizopita huku hali ya joto kali ikiendelea kukumba sehemu za nchi hiyo.

Takriban watu 33 walikufa katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh mwishoni mwa juma kutokana na joto.

Katika jimbo la Odisha (Orissa), takriban watu 20 walikufa kutokanana wimbi kali la joto, afisa aliliambia shirika la habari la ANI.

Vingi vya vifo hivi viliripotiwa tarehe 1 Juni wakati India ilipopiga kura katika awamu ya mwisho ya upigaji kura kwa uchaguzi wake mkuu.

Matokeo ya uchaguzi huo yamepangwa kutangazwa tarehe 4 Juni.

Kila baada ya miaka mitano, India hufanya uchaguzi wake mkuu katika miezi ya kiangazi ya Aprili na Mei.

Lakini mwaka huu, hali ya joto imekuwa ikivunja rekodi, huku nchi ikikumbwa na mawimbi ya joto ya mara kwa mara, makali zaidi na marefu zaidi.

Wizara ya afya ya serikali kuu inasema kwamba kumekuwa na vifo 56 vilivyothibitishwa vya mawimbi ya joto kutoka 1 Machi hadi 30 Mei. Karibu visa 24,849 mawimbi ya joto viliripotiwa katika kipindi hicho.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo