Matokeo rasmi ya uchaguzi Afrika kusini kutangazwa Jumapili
Matokeo rasmi ya uchaguzi Afrika kusini kutangazwa Jumapili
![.](https://ichef.bbci.co.uk/ace/ws/640/cpsprodpb/vivo/live/images/2024/6/1/c4b67b22-ef3c-482c-b6f8-a86b2ac860e0.jpg)
Chanzo cha picha, Reuters
Matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu Afrika kusini yanatarajiwa kutangazwa Jumapili jioni, afisa mmoja wa tume anasema.
Zoezi la kuhesabu kura linaingia katika hatua ya mwisho huku 98% ya matokeo yakiwa yamepokewa tayari.
Naibu mkurugenzi mtendaji wa tume ya uchaguzi nchini Mawethu Mosery, ameiambia televisheni ya eNCA kwamba tume itakesha usiku kucha Jumamosi kukabiliana na pingamizi na maombi.
Chama tawala ANC kinatarajiwa kupoteza nguvu kilichoshikilia katika miongo mitatu ya siasa baada ya kupungua kwa wafuasi wake kwa kiwango kikubwa.