Matokeo ya uchaguzi Afrika Kusini 2024: Zuma ataka uchaguzi urudiwe

 Zuma

Chama cha aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma kinajaribu kuzuia shughuli ya kutangaza matokeo zisifanyike kama ilivyopangwa kikitaka marudio ya uchaguzi wa juma lililopita.

Tume ya uchaguzi haitaweza kukubaliana na hili, na inasonga mbele kutangaza matokeo ya mwisho baadaye leo.

Matakwa ya chama cha MK cha Bw Zuma yanakuja ghafla.

Alikuwa mshindi mkubwa zaidi wa uchaguzi huo, akishika nafasi ya tatu katika uchaguzi wa kitaifa. Lakini alishindwa kupata wingi wa kura katika jimbo analotoka Bw Zuma la KwaZulu-Natal.

Hili ni pigo kubwa kwa chama, kwani kitalazimika kutafuta mshirika wa muungano iwapo kitataka kuliongoza jimbo hilo.

Hii inaweka kikomo chaguo la Bw Zuma la kutumia KwaZulu-Natal kama ngome ya kupigana na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, na kulazimisha kujiuzulu.

Hilo ndilo lengo kuu la Bw Zuma. Bw Ramaphosa alimtimua kama rais mwaka wa 2019, na sasa anataka kulipiza kisasi.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo