Rais wa Afrika Kusini akabiliwa na matokeo mabaya ya uchaguzi

 ,

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amekiri kuwa chama chake cha African National Congress (ANC) kimepata changamoto katika matokeo ya uchaguzi, baada ya chama hicho kupoteza wingi wa kura kwa mara ya kwanza tangu utawala wa kibaguzi kumalizika miaka 30 iliyopita.

Chama cha ANC, ambacho kiliwahi kuongozwa na Nelson Mandela, kilishinda viti 159 katika bunge lenye viti 400 katika uchaguzi wa Jumatano, idadi ya chinikutoka 230 katika bunge lililopita.

Bw Ramaphosa bado alitaja matokeo kama ushindi kwa demokrasia, akitoa wito kwa vyama vinavyopingana kutafuta muafaka - inaonekana kujiandaa kwa mazungumzo ya muungano.

Chama cha upinzani cha Democratic Alliance (DA) kimesema kiko tayari kwa mazungumzo ya muungano na Bw Ramaphosa, lakini kinapinga vipaumbele vingi vya serikali yake.

Pamoja na kura zote kuhesabiwa, ANC ilimaliza kwa kupata40% - chini kutoka 58% katika uchaguzi uliopita, tume ya uchaguzi ilitangaza Jumapili.

Hii ilikuwa chini kuliko hali ya chama inayohofiwa kuwa mbaya zaidi ya 45%, wachambuzi walisema. Chama cha ANC sasa lazima kiingie katika muungano ili kuunda serikali ijayo.

“Watu wetu wamezungumza, tupende tusitake, wamezungumza,” Bw Ramaphosa alisema.

"Kama viongozi wa vyama vya siasa, wote wanaochukua nafasi za uwajibikaji katika jamii, tumesikia sauti za watu wetu na lazima tuheshimu matakwa yao."

Aliongeza kuwa wapiga kura walitaka vyama kutafuta muafaka.

“Kupitia kura zao, wamedhihirisha wazi na wazi kwamba demokrasia yetu ni imara na inadumu,” alisema.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo