Uchaguzi Afrika Kusini: Chama cha EFF cha Julius Malema chapata pigo kubwa

 

Uchaguzi Afrika Kusini: Chama cha EFF cha Julius Malema chapata pigo kubwa

,

Chanzo cha picha, Reuters

Baada ya chama tawala cha African National Congress (ANC), aliyeshindwa zaidi katika uchaguzi huu ni chama chenye msimamo mkali cha Economic Freedom Fighters (EFF), kinachoongozwa na Julius Malema.

EFF imepoteza hadhi yake kama chama cha pili kwa ukubwa nchini Afrika Kusini kwa mshiriki wa mara ya kwanza - chama kipya cha Rais wa zamani Jacob Zuma, Umkhonto weSizwe (MK).

Huku takriban matokeo yote yakitangazwa, EFF imesimama kwa asilimia 9, chini kutoka 11 iliyopata katika uchaguzi uliopita.

Kura za MK zimesimama kwa asilimia 15, huku chama hicho kikipata kura kutoka kwa ANC na EFF.

Hili ni pigo kubwa kwa Malema na EFF.

Ana matarajio ya siku moja kuwa rais wa Afrika Kusini, na alikuwa na matumaini kwamba EFF itachukua nafasi ya pili katika uchaguzi huu, na kumfanya kuwa kiongozi wa chama kikubwa zaidi cha upinzani.

Hata hivyo, ndoto hiyo ilikatizwa na wapiga kura.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Hamas yadai kuwakamata wanajeshi wa Israel lakini Israel imekanusha madai hayo