FBI yachunguza madai kuwa Iran ilidukua kambi ya kampeni ya Trump

 

FBI yachunguza madai kuwa Iran ilidukua kambi ya kampeni ya Trump

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Shirika la Ujasusi la Marekani(FBI) limeanzisha uchunguzi kuhusu madai kuwa kambi ya kampeni ya Trump ililengwa na wadukuzi wanaofanya kazi kwa ajili ya serikali ya Iran.

"Tunaweza kuthibitisha kuwa FBI inachunguza suala hilo," shirika hilo lilisema katika taarifa fupi siku ya Jumatatu bila kumtaja rais wa zamani au Iran.

Msemaji wa kambi ya kampeni ya Trump aliiambia BBC kuwa hati hizo zilipatikana kinyume cha sheria na "vyanzo vya kigeni vinavyoichukia Marekani".

Maafisa wa Iran wamekanusha kuhusika na udukuzi huo na serikali ya Marekani haijaishutumu rasmi Iran.

FBI pia inachunguza ikiwa wadukuzi wa Iran walilenga kambi ya Joe Biden-Kamala Harris, kulingana na CBS News, mshirika wa habari wa BBC, akinukuu watu wanaofahamu uchunguzi huo.

Taarifa ya kambi ya kampeni ya Trump imetolewa siku moja baada ya Microsoft kutoa ripoti inayoonyesha kwamba wadukuzi wa Iran walilenga kampeni ya mgombea urais wa Marekani ambaye hakutajwa jina mnamo mwezi Juni.

Siku ya Jumamosi, Trump alisema wadukuzi "waliweza tu kupata habari zilizokusudiwa kutolewa kwa umma".

Kulingana na gazeti la Washington Post, wafanyikazi watatu wa kambi ya kampeni ya Biden-Harris pia walilengwa na barua pepe za ulaghai siku chache kabla ya Rais Joe Biden kutangaza kwamba anajiondoa kwenye kinyang’anyiro cha kuingia ikulu.

Msemaji wa kambi ya kampeni ya Harris alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba "wanafuatilia kwa uangalifu na kuhakikisha ulinzi dhidi ya vitisho vya mtandao, na hatufahamu ukiukaji wowote wa usalama wa mifumo yetu".

BBC imeomba kambi ya kampeni ya Harris kutoa maoni.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024