HAMAS: Hatutashiriki mazungumzo ya usitishaji vita Doha

 

  • HAMAS: Hatutashiriki mazungumzo ya usitishaji vita Doha

Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema wawakilishi wa harakati hiyo ya muqawama hawatashiriki mazungumzo ya leo ya usitishaji vita yanayotazamiwa kufanyika Doha, mji mkuu wa Qatar.

Televisheni ya Al-Mayadeen ya Lebanon jana Jumatano ilimnukuu afisa huyo wa ngazi ya juu wa HAMAS ambaye hakutaka kutaja jina lake akisema kuwa, wawakilishi wa harakati hiyo hawatahudhuria kikao cha leo Alkhamisi cha Doha, cha kujadili usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza na makubaliano ya kubadilishana mateka, kutokana na hujuma za kikatili za utawala wa Kizayuni na Waziri Mkuu wake Benjamin Netanyahu huko Gaza.

Afisa huyo wa HAMAS anasisitiza kwamba, kundi hilo la muqawama halitakubali kuanza kwa mazungumzo mapya huko Doha bila ya upande mwingine kuzingatia mapendekezo yaliyowasilishwa Julai 2. 

HAMAS Jumapili usiku wiki hii ilitoa taarifa ikisisitiza kuwa, vipengee vilivyofikiwa katika mapatano ya awali vinapasa kutekelezwa kwanza badala ya kuanza mazungumzo mapya ya kusimamisha vita huko Gaza na kuzitaka pande suluhushi kuja na mpango kwa mujibu wa mazungumzo ya awali.

Jinai za Israel katika Ukanda wa Gaza

Afisa huyo mwandamizi wa HAMAS pia ameiambia Al-Mayadeen kuwa, Netanyahu ameweka masharti mapya ambayo yatavuruga mchakato wa mazungumzo hayo. 

Hii ni katika hali ambayo, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya HAMAS awali alisema kuwa kushiriki kwao katika mazungumzo ya Doha kunategemea na kusimamishwa vita katika Ukanda wa Gaza. Yahya Sinwar ametuma ujumbe kwa ajili ya usuluhishi na akasema utawala wa Kizyauni unapasa kusitisha harakati zake za kijeshi katika Ukanda wa Gaza  kama kweli unataka kufikiwa mapatano.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China