Hamas yasema usitishaji mapigano lazima uzingatie makubaliano ya mwezi Julai
Hamas yasema usitishaji mapigano lazima uzingatie makubaliano ya mwezi Julai

Chanzo cha picha, Reuters
Hamas imesema mpango wa kusitisha mapigano Gaza lazima uzingatie wapi mazungumzo yalifanyika mwezi mmoja na nusu uliopita badala ya duru zozote mpya za mazungumzo.
Katika taarifa yake Jumapili usiku, kundi hilo lilitoa wito kwa wapatanishi "kuwasilisha mpango wa kutekeleza kile kilichokubaliwa na harakati mnamo Julai 2, 2024, kwa kuzingatia maono ya (Rais Joe Biden na azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa".
Mnamo tarehe 2 Julai, Hamas ilitoa majibu yake kwa muhtasari wa mpango wa kusitisha mapigano uliotangazwa na Bw Biden mnamo Mei 30.
Maelezo ya majibu ya Hamas hayajawekwa wazi lakini kundi hilo linaeleweka kuwa limetupilia mbali matakwa ya kusitishwa kikamilifu kwa mapigano hapo mwanzo badala ya usutishaji wa awali wa wiki sita uliotolewa na rais.
Mazungumzo yalianza tena wiki moja baadaye, huku Hamas ikiishutumu Israel kwa kuanzisha masharti mapya.