Hamas yasema usitishaji mapigano lazima uzingatie makubaliano ya mwezi Julai

 

Hamas yasema usitishaji mapigano lazima uzingatie makubaliano ya mwezi Julai

Israel ilitoa amri ya kuhama kwa wakazi wa Khan Younis kusini mwa Gaza siku ya Jumapili, kufuatia shambulio baya la anga dhidi ya shule moja katika mji wa Gaza.

Chanzo cha picha, Reuters

Hamas imesema mpango wa kusitisha mapigano Gaza lazima uzingatie wapi mazungumzo yalifanyika mwezi mmoja na nusu uliopita badala ya duru zozote mpya za mazungumzo.

Katika taarifa yake Jumapili usiku, kundi hilo lilitoa wito kwa wapatanishi "kuwasilisha mpango wa kutekeleza kile kilichokubaliwa na harakati mnamo Julai 2, 2024, kwa kuzingatia maono ya (Rais Joe Biden na azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa".

Mnamo tarehe 2 Julai, Hamas ilitoa majibu yake kwa muhtasari wa mpango wa kusitisha mapigano uliotangazwa na Bw Biden mnamo Mei 30.

Maelezo ya majibu ya Hamas hayajawekwa wazi lakini kundi hilo linaeleweka kuwa limetupilia mbali matakwa ya kusitishwa kikamilifu kwa mapigano hapo mwanzo badala ya usutishaji wa awali wa wiki sita uliotolewa na rais.

Mazungumzo yalianza tena wiki moja baadaye, huku Hamas ikiishutumu Israel kwa kuanzisha masharti mapya.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024