Hifadhi ya maiti Marekani yatozwa faini ya $950m katika kesi ya miili iliyooza
Hifadhi ya maiti Marekani yatozwa faini ya $950m katika kesi ya miili iliyooza

Chanzo cha picha, CBS
Hifadhi moja ya maiti Marekani ambapo miili 190 iliyoharibika ilipatikana imeagizwa kulipa $950m (£746m) kwa familia za waathiriwa.
Hifadhi hiyo kwa jina Return to Nature, katika mji wa Penrose, Colorado, ilikuwa imewapa jamaa waliokuwa wakiomboleza majivu bandia badala ya mabaki ya wapendwa wao.
Jaji aliamuru malipo hayo katika kesi ya madai, lakini hakuna uwezekano wa kulipwa kwa vile wamiliki wa hifadhi hiyo, Jon na Carie Hallford, walikuwa katika matatizo makubwa ya kifedha.
Wawili hao pia hawakuhudhuria vikao. Bw Hallford yuko kizuizini, huku mkewe akiwa nje kwa dhamana.
"Sitapata hata senti kutoka kwao, kwa hivyo, sijui, inasikitisha kidogo," Crystina Page, ambaye aliajiri hifadhi hiyo ya maiti i kuchoma mabaki ya mtoto wake mnamo 2019, aliiambia Associated Press.
Bi Page, ambaye alibeba kile alichodhani ni majivu ya mwanawe kwa miaka minne kabla ya mwili wake kutambuliwa nyumbani humo , pia alisema kutofika kwa wanandoa hao mahakamani kulikuwa kama 'kofi usoni'