Hifadhi ya maiti Marekani yatozwa faini ya $950m katika kesi ya miili iliyooza

Hifadhi ya maiti Marekani yatozwa faini ya $950m katika kesi ya miili iliyooza

TH

Chanzo cha picha, CBS

Hifadhi moja ya maiti Marekani ambapo miili 190 iliyoharibika ilipatikana imeagizwa kulipa $950m (£746m) kwa familia za waathiriwa.

Hifadhi hiyo kwa jina Return to Nature, katika mji wa Penrose, Colorado, ilikuwa imewapa jamaa waliokuwa wakiomboleza majivu bandia badala ya mabaki ya wapendwa wao.

Jaji aliamuru malipo hayo katika kesi ya madai, lakini hakuna uwezekano wa kulipwa kwa vile wamiliki wa hifadhi hiyo, Jon na Carie Hallford, walikuwa katika matatizo makubwa ya kifedha.

Wawili hao pia hawakuhudhuria vikao. Bw Hallford yuko kizuizini, huku mkewe akiwa nje kwa dhamana.

"Sitapata hata senti kutoka kwao, kwa hivyo, sijui, inasikitisha kidogo," Crystina Page, ambaye aliajiri hifadhi hiyo ya maiti i kuchoma mabaki ya mtoto wake mnamo 2019, aliiambia Associated Press.

Bi Page, ambaye alibeba kile alichodhani ni majivu ya mwanawe kwa miaka minne kabla ya mwili wake kutambuliwa nyumbani humo , pia alisema kutofika kwa wanandoa hao mahakamani kulikuwa kama 'kofi usoni'

 

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024