Iran yakataa wito wa nchi za Magharibi kujizuia kuishambulia Israel

 

Iran yakataa wito wa nchi za Magharibi kujizuia kuishambulia Israel

.

Chanzo cha picha, EPA

Iran imetupilia mbali wito wa Uingereza na nchi nyingine za Magharibi kujiepusha na kulipiza kisasi dhidi ya Israel kwa mauaji ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh mjini Tehran mwezi uliopita.

Huku kukiwa na msururu wa mazungumzo ya diplomasia ya kimataifa ili kupunguza mvutano, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer amemtaka Rais wa Iran Masoud Pezeshkian "kuondoa vitisho vyake vya mashambulizi ya kijeshi" katika mazungumzo ya simu yasio ya kawaida siku ya Jumatatu.

Lakini Bw Pezeshkian amesema kulipiza kisasi ni "njia ya kukomesha uhalifu" na "haki ya kisheria" ya Iran, kulingana na vyombo vya habari vya serikali ya Iran.

Israel, ambayo haikusema ilihusika katika mauaji ya Haniyeh, wakati huo huo imeweka jeshi lake katika hali ya tahadhari.

Marekani imeonya kwamba inajiandaa kwa "mashambulizi makubwa ya Iran au washirika wake wiki hii, na imejenga uwepo wake wa kijeshi katika Mashariki ya Kati ili kusaidia kuilinda Israel.

Wapiganaji wa Hezbollah wanaoungwa mkono na Iran nchini Lebanon pia wametishia kulipiza kisasi mauaji ya mmoja wa makamanda wake wakuu yaliotekelezwa na Israel katika shambulio la angani huko Beirut.

Starmer wa Uingereza anaitaka Iran kujiepusha na mashambulizi dhidi ya Israel.

Siku ya Jumatatu jioni, viongozi wa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani walitoa taarifa ya pamoja wakiitaka Iran na washirika wake "kujiepusha na mashambulizi ambayo yatazidisha mivutano ya kikanda".

"Watawajibika kwa vitendo vinavyohatarisha fursa hii ya amani na utulivu," Sir Keir, Rais Emmanuel Macron na Kansela Olaf Scholz walisema.

Baadaye, waziri mkuu wa Uingereza pia alionyesha wasiwasi wake mkubwa kupitia simu ya moja kwa moja na rais wa Iran - simu ya kwanza kama hiyo tangu Machi 2021.

Sir Kier alimwambia Bw Pezeshkian kwamba "kulikuwa na hatari kubwa ya kufanya makosa na sasa ulikuwa wakati wa utulivu na uangalifu", Downing Street ilisema.

"Alitoa wito kwa Iran kujizuia kushambulia Israeli, akiongeza kuwa vita havina maslahi ya mtu yeyote," iliongeza.

Siku ya Jumanne asubuhi, shirika la habari la serikali ya Iran Irna liliripoti kwamba Bw Pezeshkian alimwambia Sir Kier kwamba uungaji mkono wa nchi za Magharibi kwa Israel umeifanya "kuendeleza ukatili" na kutishia amani na usalama.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024