Israel na Hezbollah zafanya mashambulizi ya kujibizana huku mvutano ukizidi kupamba moto

 

srael na Hezbollah zafanya mashambulizi ya kujibizana huku mvutano ukizidi kupamba moto

th

Chanzo cha picha, IDF

Israel inasema imefanya mashambulizi ya anga dhidi ya kile ilichosema ni "jengo linalofanana kama la kijeshi" linalotumiwa na kundi la waasi la Hezbollah kusini mwa Lebanon.

Wizara ya afya ya Lebanon imesema watu wanne waliuawa katika shambulio hilo katika mji wa Maifadoun, karibu kilomita 30 kutoka mpaka wa Israel.

Vyanzo vya usalama vililiambia shirika la habari la AFP kwamba watu hao wanne walikuwa wapiganaji wa Hezbollah. Katika jibu dhahiri, kundi hilo lilianzisha mashambulizi ya ndege zisizo na rubani kwenye miji ya kaskazini mwa Israel, na kuwajeruhi watu wawili.

Inakuja huku kukiwa na mvutano unaoongezeka kati ya Israel na Hezbollah, na Iran ambayo inaunga mkono kundi hilo.

Wiki iliyopita, shambulio la anga la Israel lilimuua kamanda mwandamizi wa Hezbollah Fuad Shukr katika kitongoji cha kusini mwa mji mkuu wa Lebanon Beirut, katika kile maafisa wa Israel walichokiita "kutokomeza kwa kutegema habari za kijasusi".

Maafisa wa Israel wanasema alihusika na shambulio la roketi katika eneo la Milima ya Golan inayokaliwa na Israel mwezi uliopita na kuua watoto na vijana 12. Hezbollah imekanusha kuhusika na shambulio hilo.

Saa chache baada ya Shukr kuuawa, kiongozi wa kisiasa wa Hamas Ismail Haniyeh aliuawa katika mji mkuu wa Iran Tehran - Iran ililaumu Israel kwa shambulio hilo .

Hezbollah na Iran zimeapa kulipiza kisasi juu ya vifo hivyo, na hivyo kuzua hofu kwamba mapigano ya kujibizana yanaweza kuchochea mzozo mkubwa zaidi wa kikanda.

Nchi kadhaa, ikiwa ni pamoja na Marekani, zimewataka raia kuondoka Lebanon haraka iwezekanavyo. Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo alisema Jumanne kwamba alikuwa anafanya kazi kuhakikisha kuwa Hezbollah haisababishi ongezeko kubwa la jibu lake kutokana na kifo cha Shukr.

Shambulio la Israel dhidi ya Maifadoun lilitekelezwa na ndege za kivita, na liliongozwa na mashirika ya kijasusi, Jeshi la Ulinzi la Israel lilisema katika taarifa iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii.

Kujibu, Hezbollah ilifyatua kile ilichokiita "kundi" la ndege zisizo na rubani dhidi ya Israel, na kuwajeruhi watu wawili katika mji wa kaskazini wa Mazra'a. Lakini chanzo katika kundi hilo kililiambia shirika la habari la Reuters kwamba shambulio hilo halikuwa sehemu ya majibu yake kwa kifo cha Shukr.

Rais wa Marekani Joe Biden alikutana na timu yake ya juu ya usalama wa taifa siku ya Jumatatuhuku wasiwasi wa mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya Israel ukiongezeka.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024