Jeshi la Sudan lasusia mazungumzo ya amani yanayoongozwa na Marekani

 

Jeshi la Sudan lasusia mazungumzo ya amani yanayoongozwa na Marekani

Mkuu wa jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan alikataa kutuma ujumbe kwenye mazungumzo ya amani huko Geneva.

Chanzo cha picha, AFP

Mazungumzo mapya ya amani yenye lengo la kumaliza vita vya miezi 16 vya Sudan yameanza licha ya moja ya pande zinazopigana, jeshi la taifa, kukataa kuhudhuria.

Marekani, ambayo inawezesha majadiliano, ilisisitiza kuwa tukio hilo liliendelea bila kujali kama mamilioni ya watu wanaoteseka nchini Sudan "hawawezi kumudu kusubiri".

Mapigano kati ya jeshi na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) yamegharimu maelfu ya maisha, na kusababisha watu takribani milioni 10 kukimbia makazi yao.

Jeshi lilikatiza matumaini ya makubaliano ya kusitisha mapigano kwa kususia mazungumzo ya Jumatano, likisema kwamba halitahudhuria kwa vile RSF haikutekeleza "kile kilichokubaliwa" nchini Saudi Arabia mwaka jana.

RSF haikuwa imetimiza masharti muhimu ya Azimio la Jeddah, kama vile kuwaondoa wapiganaji wake kutoka kwenye nyumba za raia na vituo vya umma, jeshi lilisema.

Katika taarifa kwenye mtandao wa kijamii wa X, RSF ilisema imefika katika mji wa Uswizi wa Geneva kwa mazungumzo na kutoa wito kwa jeshi "kujitolea kutimiza matarajio ya kidemokrasia ya watu wa Sudan".

Jeshi pia lilikataa mazungumzo hayo kwa vile linapinga kuwepo kama mwangalizi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), ambayo inashutumu kuunga mkono RSF.

Kando ya UAE, wajumbe wanaowakilisha Marekani, Saudi Arabia, Misri, Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa wanahudhuria.

Kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji, makumi ya maelfu ya vifo vinavyoweza kuzuilika vinakaribia nchini Sudan ikiwa mzozo na vikwazo vya misaada ya kibinadamu vitaendelea.

Marekani ilisema mzozo huo umefikia kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kushuhudiwa huku mamilioni ya watu wakikabiliwa na njaa na kuyahama makazi yao.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Putin asaini mkataba wa kituo cha Mwezi na China