Mahojiano ya Trump na Musk yakumbwa na changamoto za kiufundi
Mahojiano ya Trump na Musk yakumbwa na changamoto za kiufundi

Chanzo cha picha, X/Reuters
Mjadala uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu kati ya Elon Musk na mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump kwenye jukwaa la bilionea la X, ulighubikwa na changamoto za kiufundi.
Mazungumzo hayo, ambayo Bw Musk aliuliza maswali ya kirafiki kuhusu mada kama vile uhamiaji na mfumuko wa bei, dakika 40 baadaye tangu muda uliokuwa umepangwa kuanza, huku watumiaji wengi wakihangaika kuyafikia.
Ilichukuliwa kama mahojiano lakini Trump alitoa mfululizo wa madai ambayo hayajathibitishwa na hayakupingwa na yeyote.
Bw Musk alirudia kumuunga mkono Trump, ambaye atakabiliana na mgombea mpya wa chama cha Democratic, Makamu wa Rais Kamala Harris, katika uchaguzi wa Novemba.
Alilaumu changamoto hizo za kiufundi kutokana na uvamizi wa mtandao lakini mtaalamu mmoja aliambia BBC kwamba hilo haliwezekani.