Mkuu wa Umoja wa Mataifa ataka Afrika ipewe kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la UN

 

Mkuu wa Umoja wa Mataifa ataka Afrika ipewe kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la UN

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Gutierrez

Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa Afrika kupewa kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kama sehemu ya mageuzi ya kurekebisha dhuluma za kihistoria.

Baraza la Usalama lenye - wanachama watano wa kudumu ambao ni China, Ufaransa, Urusi, Uingereza na Marekani – kwa muda mrefu limekuwa likikosolewa kwa kuwakilisha hali halisi iliyokuwepo mwishoni mwa Vita vya Pili vya Dunia wakati sehemu kubwa ya Afrika ilikuwa bado chini ya ukoloni.

"Ulimwengu umebadilika tangu 1945. Lakini muundo wa Baraza, licha ya mabadiliko machache, haujabadilika," Bw Guterres alisema.

Wajumbe 10 wasio wa kudumu wa baraza hilo wanawakilishwa kikanda, lakini tofauti na wajumbe watano wa kudumu, hawana uwezo wa kura ya turufu.

Umoja wa Afrika kwa muda mrefu umekuwa ukishinikiza bara la Afrika kuwa na wawakilishi wawili wa kudumu katika baraza hilo na viti vingine viwili kama wawakilishi wasio wa kudumu.

Mjadala wa Jumatatu uliitishwa na Sierra Leone - na Rais wake Julius Maada Bio aliwakilisha hoja ya bara hilo."

''Wakati wa hatua nusu za maendeleo ya ziada umekwisha. Afrika lazima isikizwe, na matakwa yake ya haki na usawa lazima yatimizwe,” alisema.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina majukumu makubwa, ikiwa ni pamoja na kuidhinisha operesheni za ulinzi wa amani, kuweka vikwazo vya kimataifa na kuamua jinsi UN inapaswa kukabiliana na migogoro kote duniani.

Maafisa wengine wa Umoja wa Mataifa waliunga mkono maoni ya mageuzi, akiwemo Dennis Francis - rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, pamoja na Bw Guterres.

"Hatuwezi kukubali kwamba chombo kikuu cha amani na usalama duniani hakina sauti ya kudumu kwa bara lenye zaidi ya watu bilioni moja –Lenye idadi ya vijana na inayokua kwa kasi - ambayo ni asilimia 28 ya wanachama wa Umoja wa Mataifa," mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa alisema.

.Afrika ilikuwa na uwakilishi mdogo katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na taasisi za fedha za kimataifa lakini "iliwakilishwa kupita kiasi katika changamoto ambazo miundo hii imeundwa kushughulikia", aliongeza.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024