Putin: 'Lazima tumfukuze adui nje ya eneo letu
Putin: 'Lazima tumfukuze adui nje ya eneo letu

Chanzo cha picha, Reuters
Tumekuwa tukipata maelezo kutoka Urusi - ambapo Rais Vladimir Putin ameitisha mkutano wa maafisa kuhusu hali katika mikoa ya mpakani.
Anauambia mkutano huo unaoenda moja kwa moja hewani katika runinga ya serikali kwamba "kazi kuu ya wizara ya ulinzi ni kusukuma, kuwafukuza adui kutoka katika eneo letu".
Pia anasema kuwa lengo la Ukraine katika shambulio hilo ilikuwa kuboresha nafasi yake ya mazungumzo.