Saa 1 iliyopitaMaandamano Bangladesh: Tunachokijua kufikia sasa

 

Maandamano Bangladesh: Tunachokijua kufikia sasa

Muandamanaji

Chanzo cha picha, Reuters

Kuna hali ya sintofahamu miongoni mwa wananchi wengi wa Bangladesh kuhusu kitakachotokea baadaye, siku moja baada ya Waziri Mkuu Sheikh Hasina kulazimishwa kujiuzulu na kuikimbia nchi kufuatia maandamano makubwa.

Hasina, 76, anaaminika kuwa bado yuko katika nchi jirani ya India, lakini uvumi umeenea kwamba anaweza kuwa anajiandaa kwenda katika nchi nyingine ya kigeni.

Siku ya Jumatatu, mkuu wa jeshi la Bangladesh aliahidi kwamba serikali ya mpito itaundwa hivi karibuni, lakini hakutoa maelezo kuhusu nani anaweza kuiongoza. Viongozi wa wanafunzi wanasema hawatakubali serikali inayoongozwa na jeshi, wakishinikiza mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Muhammad Yunus kuwa mshauri mkuu wa baraza jipya la mawaziri.

Baadhi yao wamemtaka rais wa Bangladesh Mohammed Shahabuddin kulivunja bunge ifikapo saa 15:00 kwa saa za huko leo (09:00 GMT), na wameonya kwamba "watachukua hatua kali" ikiwa matakwa yao hayatatekelezwa.

Endelea kuwa nasi tunapokuletea habari za hivi punde na uchambuzi kutoka Bangladesh.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024